Thursday 31 December 2009

Portsmouth 1 Arsenal 4
Timu iliyo mkiani kwenye Ligi Kuu, Portsmouth, leo uwanjani kwao Fratton Park wamezidi kupigiliwa misumari huko chini baada ya kupata kichapo cha mabao 4-1 toka kwa Arsenal kwenye mechi ya Ligi Kuu.
Kwa ushindi huu, Arsenal wamefikisha pointi 41 kwa mechi 19 na wako nafasi ya 3 wakiwa nyuma ya Man U walio nafasi ya pili wakiwa na pointi 43 kwa mechi 20.
Hadi mapumziko Arsenal ilikuwa mbele kwa bao 2 Wafungaji wakiwa Eduardo, dakika ya 27 na Nasri dakika ya 42.
Kipindi cha pili Arsenal wakaongeza bao 2 kupitia Ramsey na Song.
Bao la Portsmouth lilifungwa na Nadir Belhadj.
VIKOSI:
Portsmouth: Begovic, Finnan, Kaboul, Ben-Haim, Hreidarsson, Yebda, Mokoena, Hughes, Belhadj, Boateng, Piquionne.
AKIBA: Ashdown, Diop, Brown, Utaka, Vanden Borre, Kanu, Wilson.
Arsenal: Almunia, Sagna, Gallas, Vermaelen, Traore, Ramsey, Song Billong, Diaby, Nasri, Eduardo, Arshavin.
AKIBA: Fabianski, Rosicky, Vela, Silvestre, Wilshere, Merida, Eastmond.

No comments:

Powered By Blogger