Sunday 27 December 2009

Man U yaidunda Hull na kurudi nafasi ya 2!!!
Kwa mara ya kwanza katika mechi karibu 5, Manchester United leo walishuka ugenini uwanja wa KC kupambana na Hull City kwenye mechi ya Ligi Kuu huku wakiwa na Difensi ambayo inatambulika na si ile ya kuungaunga iliyowafanya wachapwe na Villa na Fulham.

Leo Beki ilichezwa na Rafael pembeni kulia, Evra pembeni kushoto na Dabo Sentahafu ilichezwa na Wes Brown na Nemanja Vidic.
Carrick na Fletcher ambao ndio walikuwa wakicheza kama Masentahafu katika mechi za hivi karibuni, kwenye mechi hii walirudi kwenye nafasi zao za kawaida za Kiungo.
Na Kikosi hicho kilichokuwa na uwiano hakikuwaangusha Washabiki wa Man U kwani waliibuka na ushindi wa mabao 3-1 na hivyo kuipiku Arsenal na kutinga nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi huku Chelsea bado wakiongoza wakiwa na pointi 42, Man U 40, Arsenal 38 na Aston Villa 35. 
Wayne Rooney alifunga bao la kwanza Kipindi cha Kwanza kwenye dakika za majeruhi baada ya kazi nzuri kwenye wingi ya kulia ya Darren Fletcher alietia krosi iliyoguswa na Giggs na kumkuta Rooney alieidokoa hadi wavuni.
Kipindi cha pili Hull walisawazisha kwa penalti iliyofungwa na Craig Fagan dakika ya 14 baada ya pasi ya Rooney kunaswa na Fagan aliempasia Jozy Altidore ambae aliangushwa na Rafael wa Man U na Refa Alan Wiley kuamua ni penalti.
Katika dakika ya 28 ya Kipindi hicho cha Pili, Man U walifunga bao la pili baada ya Giggs kumpenyezea Rooney aliepiga krosi ili imfikie Park [alieingizwa badala ya Valencia] lakini Beki wa Hull Andy Dawson akajifunga mwenyewe.
Dimitar Berbatov akaweka wavuni bao dakika ya 82 baada ya pande tamu kutoka kwa Wayne Rooney.
VIKOSI:
Hull: Myhill, Mendy, Gardner, Zayatte, Dawson, Garcia, Boateng, Olofinjana, Hunt, Altidore, Fagan.
AKIBA: Duke, Barmby, Geovanni, Kilbane, Ghilas, Vennegoor of Hesselink, Cairney.
Man Utd: Kuszczak, Rafael Da Silva, Vidic, Brown, Evra, Valencia, Carrick, Fletcher, Giggs, Berbatov, Rooney.
AKIBA: Foster, Owen, Park, Welbeck, Fabio Da Silva, Obertan, De Laet.
REFA: Alan Wiley
MECHI ZINAZOKUJA ZA LIGI KUU England: [saa za bongo]
Jumatatu, 28 Desemba 2009
[saa 9 dak 45 mchana]
Tottenham v West Ham
[saa 12 jioni]
Blackburn v Sunderland
Chelsea v Fulham
Everton v Burnley
Stoke v Birmingham
[saa 4 dak 45 usiku]
Wolves v Man City
Jumanne, 29 Desemba 2009
[saa 4 dak 45 usiku]
Aston Villa v Liverpool
[saa 5 usiku]
Bolton v Hull
Jumatano, 30 Desemba 2009
[saa 4 dak 45 usiku]
Portsmouth v Arsenal
[saa 5 usiku]
Man U v Wigan

No comments:

Powered By Blogger