Sunday 31 January 2010

Man United: ‘Rooney hauzwi kwa bei yeyote ile!!’
Mkurugenzi Mtendaji wa Manchester United, David Gill, ametamka kuwa Straika wao Wayne Rooney hauzwi kwa bei yeyote ile.
Msimu huu Rooney ni moto wa kuotea mbali na tayari ameshafunga jumla ya mabao 21 na kwenye Ligi Kuu yeye ndie anaeongoza kwa ufungaji.
Kumekuwa na tetesi kuwa Klabu za Spain Real Madrid na Barcelona zinamnyemelea Rooney.
David Gill amesema: “Labda atake Meneja wake Sir Alex Ferguson, lakini sisi hatukubali ofa yeyote kwake! Sisi tunataka abaki hapa!”
Vile vile, David Gill aliwapoza Mashabiki wenye wasiwasi kuwa Man United hamna pesa za kununua Wachezaji kwa kutoboa kuwa Klabu hiyo ilitoa ofa ya Euro Milioni 35 kumnunua Karim Benzema lakini ofa hiyo ikakataliwa na Mchezaji huyo akanunuliwa na Real Madrid kwa zaidi ya Euro Milioni 40 kiwango ambacho David Gill amesema Sir Alex Ferguson aliona ni kikubwa mno.
Gill alisistiza kuwa Rooney ana mkataba hadi 2012 na mwishoni mwa msimu huu mazungumzo yataanza na Wawakilishi wa Rooney ili kuuboresha na kuurefusha mkataba wake.
Katika dirisha la uhamisho la Januari Man United imemnunua Mlinzi Chipukizi Chris Smalling, miaka 20, kutoka Fulham kwa dau linalokadiriwa kuwa Pauni Milioni 7 na Mchezaji huyo ameachwa aendelee Fulham hadi mwishoni mwa msimu.

No comments:

Powered By Blogger