Friday 5 February 2010

Droo ya UEFA EURO 2012 ni Jumapili!!!
Mabingwa Watetezi Spain ni miongoni mwa Nchi 9 zilizoteuliwa kuwemo kwenye Kapu la Kwanza la Miamba, na hivyo kuzitenganisha Nchi kubwa kutokutana katika mechi za awali za mtoano, katika droo ya kupanga Makundi ya raundi za mtoano za UEFA EURO 2012 Mashindano ambayo yanashirikisha Mataifa ya Ulaya.
Droo hiyo inafanyika Jumapili Februari 7 huko Mjini Warsaw, Poland.
Fainali za UEFA EURO 2012 zitafanyika katika Nchi mbili, Poland na Ukraine kwa pamoja, na itashirikisha jumla ya Nchi 16.
Wenyeji Poland na Ukraine wameingizwa Fainali moja kwa moja.
Katika droo hiyo Timu zimegawanywa katika Makapu 6 na zitapangwa katika Makundi 9 kugombea nafasi 14 za kuingia Fainali kujumuika na Poland na Ukraine.
Washindi wa kila Kundi pamoja na Timu moja iliyo nafasi ya Pili yenye matokeo bora kuliko wengine zitaingia Fainali. Washindi wa pili wengine wanane watapangiwa mechi nyngine maalum za mtoano ili kupata Timu za mwisho 4.
Mechi katika Makundi, zikichezwa kwa mtindo wa Ligi wa nyumbani na ugenini, zitachezwa kati ya Septemba, 2010 na Oktoba, 2011.
KAPU 1: Spain (Mabingwa Watetezi), Germany, Netherlands, Italy, England, Croatia, Portugal, France, Russia
KAPU 2: Greece, Czech Republic, Sweden, Switzerland, Serbia, Turkey, Denmark, Slovakia, Romania
KAPU 3: Israel, Bulgaria, Finland, Norway, Republic of Ireland, Scotland, Northern Ireland, Austria, Bosnia-Herzegovina
KAPU 4: Slovenia, Latvia, Hungary, Lithuania, Belarus, Belgium, Wales, FYR Macedonia, Cyprus
KAPU 5: Montenegro, Albania, Estonia, Georgia, Moldova, Iceland, Armenia, Kazakhstan, Liechtenstein
KAPU 6: Azerbaijan, Luxembourg, Malta, Faroe Islands, Andorra, San Marino

No comments:

Powered By Blogger