Saturday 6 February 2010

TATHMINI MECHI ZA WIKIENDI LIGI KUU:
Gumzo na hamu kubwa ya Wadau wengi, bila shaka, wikiendi hii italenga Dabi ya Liverpool ya Jumamosi inayowakutanisha Wapinzani wa Jadi Liverpool v Everton Uwanjani Anfield na ile Bigi Mechi itakayochezwa Stamford Bridge kati ya Chelsea na Arsenal.
Kwingineko katika wikiendi hii ambayo Timu zote 20 za Ligi Kuu zimo dimbani tutashuhudia Timu iliyo mkiani na ambayo ipo kwenye majaribu makubwa ya matatizo ya fedha yakichanganyika na Wamiliki kubadilika kila kukicha na pia ripoti za Meneja kukutwa kwenye danguro, Timu ya Portsmouth, ikiingia kwenye mdomo wa simba pale itakaposhuka Old Trafford kupambana na Bingwa Manchester United.
Pia kuna mechi tamu kati ya Tottenham na Aston Villa mechi inayozikutanisha Timu zinazogombea nafasi ya 4 ambayo ni muhimu kwa kucheza UEFA CHAMPIONS LEAGUE msimu ujao.
Saa ni za Bongo.
JUMAMOSI, FEBRUARI 6
Liverpool v Everton [Anfield, saa 9 dak 45 mchana]
Wikiendi ya Ligi Kuu itafunguliwa rasmi Jumamosi kwa pambano la saa 9 dakika 45 mchana la Mahasimu Liverpool na Everton.
Everton, wakiwa chini ya Meneja David Moyes, hawajafungwa katika mechi 9 za Ligi na wameshinda mechi 4 katika 5 zao za mwisho. Mara ya mwisho Everton kufungwa kwenye Ligi ilikuwa ni Novemba walipofungwa na Liverpool 2-0.
Liverpool wapo pointi 9 mbele ya Everton na fomu yao kwenye Ligi imekuwa haitabiriki na hilo litalifanya pambano hili kuwa tamu.
Everton huenda ikwachezesha Mikael Arteta, aliekuwa majeruhi muda mrefu, na Joseph Yobo, aliekuwa Angola na Nigeria kwenye Kombe la Mataifa ya Afrika. Lakini Everton itawakosa majeruhi Tony Hibbert na Phil Jagielka.
Liverpool itawakosa majeruhi Fernando Torres, Yossi Benayoun na Glen Johnson.
Vikosi vinategemewa kuwa:
Liverpool (4-2-3-1): Reina; Carragher, Skrtel, Kyrgiakos, Insua; Aquilani, Mascherano; Kuyt, Gerrard, Riera; Ngog.
Everton (4-4-1-1): Howard; Neville, Heitinga, Senderos, Baines; Donovan, Fellaini, Osman, Pienaar; Cahill; Saha.
Refa: Martin Atkinson
Manchester United v Portsmouth [Old Trafford, saa 12 jioni]
Huko Old Trafford, Manchester United wakitoka freshi kwenye ushindi mnono walioupata Emirates walipoichabanga Arsenal 3-1 wana nafasi kubwa ya kuwa kileleni mwa Ligi Kuu ikiwa wataifunga Portsmouth Timu iliyo mkiani kwa sababu Chelsea wanaoongoza Ligi kwa pointi mbili wanacheza Jumapili.
Man United itakuwa bila ya Rio Ferdinand anaetumikia kifungo cha mechi 4 hii ikiwa ni mechi yake ya pili. Pia majeruhi Owen Hargreaves, Nemanja Vidic na John O’Shea hawatakuwepo.
Portsmouth watawakosa Michael Brown na Papa Bouba Diop walioumia lakini Mchezaji mpya Riccardo Rocha huenda akacheza.
Vikosi vinategemewa:
Manchester United (4-3-3): Van der Sar; Fabio, Evans, Brown, Evra; Scholes, Carrick, Fletcher; Nani, Rooney, Park.
Portsmouth (4-3-3): James; Finnan, Ben-Haim, Rocha, Belhadj; Yebda, Basinas, Boateng, O’Hara; Dindane, Piquionne.
Refa: Lee Mason.
Hull City v Manchester City [KC Stadium, saa 12 jioni]
Baada ya kuisimamisha Chelsea hapo juzi Uwanja huo huo wao wa KC, Hull City watategemea matokeo mazuri tena watakapoivaa Manchester City.
Hull City wako nafasi ya 18 wakifungana na Timu nyingine tatu wote wakiwa na pointi 21 na chochote watakachopata kitawasaidia kujinasua toka chini.
Sunderland v Wigan Athletic [Stadium of Light, saa 12 jioni]
Ni mechi ya Timu zilizo kwenye kipindi cha matokeo mabovu kwao. Timu hizi mbili, kati yao, zimecheza jumla ya mechi 18 na kushinda moja tu.
Sunderland wako nafasi ya 13 wakiwa pointi mbili juu ya Wigan.
Bolton Wanderers v Fulham [Reebok Stadium, saa 12 jioni]
Baada ya vipigo vitano mfululizo, Fulham walishinda hapo juzi walipoipiga Portsmouth 1-0 huo ukiwa ushindi wao wa kwanza tangu walipoifunga Man United mapema Desemba mwaka jana.
Bolton wako nafasi ya 16 wakiwa na pointi 21 na matokeo yao kwa mechi za nyumbani si mazuri sana kwani wameshinda mechi 3 kati ya 12 walizocheza Reebok.
Burnley v West Ham [Turf Moor, saa 12 jioni]
Burnley wako nafasi ya 19 ikiwa ni juu tu ya Portsmouth walio mkiani lakini wako pointi moja tu nyuma ya wapinzani wao West Ham walio nafasi ya 15 na takwimu hizi zinaonyesha vita ilivyo kali kwa Timu za chini zinazopigana kujinusuru kushuka Daraja.
Hii ni Bigi Mechi kwa Timu hizi mbili katika vita hiyo.
West Ham, chini ya Meneja Gianfranco Zola, wameimarisha Kikosi chao katika dirisha la uhamisho la Januari na sasa wana Mastraika watatu wapya ambao huenda wakashushwa uwanjani.
Nao ni Mido, Benni McCarthy na Ilan.
Burnley wako chini ya Meneja mpya Brian Laws na hii ni mechi yake ya 4 tangu ashike wadhifa huo na zote 4 wamefungwa.
Ni mechi muhimu sana kwake.
Stoke City v Blackburn Rovers [Britannia, saa 12 jioni]
Timu hizi mbili zimeibuka upya katika mechi zao za mwisho na hazijafungwa katika mechi 3 za mwisho. Blackburn wako nafasi ya 11 wakiwa na pointi 28 na Stoke wako nafasi ya 12 na wana pointi 26.
Tottenham v Aston Villa [White Hart Lane, saa 2.30 usiku]
Pambano jingine tamu la Jumamosi ni lile la Timu mbili zinazowania nafasi ya 4, Tottenham v Aston Villa. Timu hizi zilikutana mwezi Novemba na kutoka suluhu. Kwa sasa Tottenham ndio wanaoshikilia nafasi ya 5 lakini Villa wako pointi 2 nyuma huku wana mechi moja mkononi.
JUMAPILI, FEBRUARI 7
Birmingham v Wolverhamton Wanderers [Molineux, saa 10.30]
Hii ni mechi ya kwanza ya Jumapili kabla ya ile Bigi Mechi Chelsea v Arsenal.
Hii ni mechi kati ya Timu zenye takwimu tofauti kabisa.
Birmingham wako nafasi ya 8 wakiwa na pointi 34 na wamefungwa mechi moja tu kati ya 14 walizocheza mwisho lakini kati ya hizo 14 wameshinda moja tu.
Wolves wako nafasi ya 17 na wana pointi 21.
Chelsea v Arsenal [Stamford Bridge, saa 1 usiku]
Pambano hili la Stanford Bridge ambalo limebatizwa 'Bigi Mechi' limegubikwa na kashfa ya Nahodha wa Chelsea John Terry ambae tayari ameshatimuliwa kama Nahodha wa England hapo jana.
Hata hivyo hili ni pambano muhimu kwani linakutanisha Timu iliyo nafasi ya kwanza na ya 3 huku Manchester United akitishia kuwapiku na kuchukua nafasi ya juu na pengine huenda akaipata kwani wakati mechi hii inachezwa Jumapili, Man United anacheza Jumamosi na akiifunga Portsmouth atakwea kilele na atabaki huko ikiwa Arsenal itaifunga Chelsea.
Kwa Arsenal, huu ni wakati mgumu na hili ni pambano gumu na la muhimu sana kwani mechi mbili za nyuma ya hii walitoka sare na Aston Villa na wakafungwa na Man United. Leo wako na Chelsea na Jumatano Liverpool iko mbele yao.
Hakika, ni wakati mgumu mno kwa The Gunners.
Chelsea watacheza bila ya majeruhi Juliano Belletti na Michael Essien lakini wale Cole wawili, Ashley Cole na Joe Cole, walioanza benchi mechi ya juzi na Hull City, huenda wakaanza mechi hii.
Arsenal bado itawakosa majeruhi wao Van Persie, Eduardo na Abou Diaby lakini huenda Nicklas Bendtner akashiriki.
Takwimu muhimu sana kwa Wadau wa mechi hii ni ile ya Refa atakaechezesha.
Refa Mike Dean katika mechi 16 za Ligi Kuu alizochezesha ametoa penalti 11.
Vikosi vinategemewa:
Chelsea (4-3-1-2): Cech; Ivanovic, Carvalho, Terry, A Cole; Kalou, Lampard, J Cole; Ballack; Anelka, Drogba.
Arsenal (4-3-3): Almunia; Sagna, Gallas, Vermaelen, Clichy; Fabregas, Song, Denilson; Nasri, Bendtner, Arshavin.
Refa: Mike Dean

No comments:

Powered By Blogger