Saturday 6 February 2010

Liverpool 1 Everton 0
Dirk Kuyt aliipa ushindi Liverpool alipopachika bao kwa kichwa kufuatia kona dakika ya 55 katika Dabi ya Jiji la Liverpool iliyoisha huku kila Timu ina Mtu 10 baada ya Kyrgiakos wa Liverpool na Pienaar kupewa Kadi Nyekundu katika nyakati tofauti.
Mechi hii ilitawaliwa na rafu nyingi na Refa Martin Atkinson alitembeza Kadi nyingi za Njano.
Vikosi vilivyoanza:
Liverpool: Reina, Carragher, Kyrgiakos, Agger, Insua, Mascherano, Lucas, Kuyt, Gerrard, Maxi, Ngog.
Akiba: Cavalieri, Aquilani, Riera, Aurelio, Babel, Degen, Skrtel.
Everton: Howard, Neville, Distin, Heitinga, Baines, Fellaini, Donovan, Osman, Cahill, Pienaar, Saha.
Akiba: Nash, Bilyaletdinov, Arteta, Yakubu, Senderos, Anichebe, Coleman.
Refa: Martin Atkinson
Saha na ulaji mpya Everton!!
Fowadi wa Everton Louis Saha, miaka 31, amesaini mkataba mpya wa miaka miwili na Klabu yake na hivyo kuondoa utata kuwa anaondoka.
Saha alijiunga na Everton mwaka 2008 akitokea Manchester United na msimu huu amekuwa moto mkali kwa kufunga mabao na mpaka sasa ana mabao 13.
Ilidaiwa kuwa Klabu za Bordeaux ya Ufaransa, Besiktas yaa Uturuki na AS Roma ya Italy zilikuwa zikimuwinda.
Hargreaves kurudi kutetea Ubingwa
Sir Alex Ferguson amesema Owen Hargreaves anaweza kucheza mechi za baadae za Ligi Kuu ingawa bado mpaka sasa haijajulikana lini atakuwa fiti kabisa kucheza.
Hargreaves hajacheza tangu Septemba 2008 na baada ya hapo akafanyiwa upasuaji katika magoti yake yote mawili yaliyokuwa na maumivu.
Hargreaves hakuingizwa kwenye Kikosi cha Wachezaji 25 cha Man United kilichosajiliwa UEFA kwa ajili ya mechi za Mtoano za UEFA CHAMPIONS LEAGUE.
Ferguson amesema: “Owen atarudi tu. Anaweza kucheza Ligi na kutusaidia sana. Ligi ina mechi nyingi kupita UEFA na sihitaji kumsajili kwa ajili ya Ligi.”

No comments:

Powered By Blogger