Thursday 4 February 2010

Meneja Pompey akutwa danguro!!!
Wakati Klabu yake Portsmouth iko majaribuni kwa ukosefu wa fedha huku ikiwa imepata Mnunuzi mpya wa 4 katika mwaka mmoja, zimeibuka ripoti kuwa Meneja wao Avram Grant ambae ni raia wa Israel alikutwa kwenye danguro Desemba 18 mwaka jana na alipohojiwa na Mwandishi wa Habari wakati akitoka humo ndani ya danguro alikokaa kwa muda wa saa moja, Grant alikubali hilo ni danguro lakini alikataa kusema alikwenda kufanya nini.
Ingawa habari za kwamba Meneja wa Klabu ya Ligi Kuu akutwa danguroni zilijulikana wakati huo huo, jina na Klabu yake halikutajwa kwa kuogopa sheria lakini tangu Mahakama ifute amri za kutotaja majina kwenye kesi iliyomhusu John Terry, Magazeti yamepata uhuru kuyataja na ndio maana sasa jina la Grant limetajwa waziwazi.
Danguro hilo lipo jirani tu na Uwanja wa mazoezi wa Portsmouth na linaendeshwa kwa kisingizio cha mahala pa kukanda na kuchua watu.
Huko Uingereza ukahaba si kosa na kumtumia kahaba katika mahali pa faraha si kosa pia lakini kuendesha danguro ni kosa na hukumu yake ni miaka 7 jela.

No comments:

Powered By Blogger