Wednesday 3 February 2010

LIGI KUU England: Hull City 1 Chelsea 1
Hull City walikipiga kiume na kuisimamisha Chelsea kwa kutoka droo ya 1-1 katika mechi ya LigI kuu iliyochezwa Uwanja wa KC hapo jana na hivyo kuwazuia vinara wa Ligi Chelsea kuongeza uongozi wao wa Ligi kuwa pointi 4 mbele ya Timu ya Pili Manchester United.
Kwa matokeo hayo, msimamo wa Ligi huko kileleni ni:
[Timu zimecheza mechi 24 isipokuwa inapotajwa]
1 Chelsea pointi 55
2 Man Utd pointi 53
3 Arsenal pointi 49
4 Tottenham pointi 42
5 Liverpool pointi 41
6 Manchester City pointi 41 [mechi 22]
7 Aston Villa pointi 40 [mechi 23]
Hull City ndio walipata bao la kwanza kupitia Steven Mouyokolo aliefunga kwa kichwa dakika ya 30.
Didier Drogba akicheza mechi yake ya kwanza tangu arudi toka Angola alikoichezea Nchi yake Ivory Coast kwenye Kombe la Mataifa ya Afrika alisawazisha kwa frikiki muda mfupi kabla haftaimu.
Ingawa Hull City wamepata pointi moja kwenye mechi hii lakini bado wako kwenye lile eneo la hatari la Timu 3 za chini zinazoporomoka Daraja.
Hull City wako nafasi ya 18 wakiwa juu tu ya Burnley na Timu iliyo mkiani Portsmouth.
MECHI YA LIGI KUU LEO jumatano Februari 3:
[saa 5 usiku, saa za bongo]
Fulham v Portsmouth
Licha ya kuchelewa Uhamisho, Benjani aruhusiwa na FA!!!
Mchezaji kutoka Zimbabwe, Benjani Mwaruwaru, ameruhusiwa na FA kuhama kwa mkopo kutoka Manchester City kwenda Sunderland licha ya makabrasha yake ya uhamisho kuchelewa kufika FA na kupokelewa Masaa 23 baada ya dirisha la uhamisho kufungwa hapo Jumatatu Februari 1.
FA ilichunguza na kuridhika kuwa matatizo ya kiufundi ndio yaliyosababisha barua pepe za uhamisho wa Benjani kuchelewa kuwafikia kwa wakati na hivyo kuubariki uhamisho huo.
Kwa Benjani Sunderland ni Klabu yake ya 3 kuichezea kwenye Ligi Kuu England baada ya kuwepo Portsmouth na Manchester City.
Meneja wa Sunderland, Steve Bruce, akiwa mwenye furaha alisema: “Ni jitu kubwa lenye nguvu na ni Sentafowadi tuliemtaka siku nyingi!”

No comments:

Powered By Blogger