Tuesday 2 February 2010

LIGI KUU England: Leo vinara Chelsea wako KC!!!
Timu inayoongoza Ligi Kuu, Chelsea, leo wako ugenini Uwanja wa KC nyumbani kwa Hull City ambao hali yao ni taaban kwenye Ligi hiyo na wako nafasi ya 19 ikiwa ni nafasi moja toka mkiani.
Chelsea, kama kawaida, wataongozwa na Nahodha wao John Terry ambae kwa sasa anasakamwa na skandali la kutembea na gelfrendi wa Mchezaji mwenzake wa Chelsea wakati huo, Wayne Bridge, lakini hilo halikumzuia katika mechi iliyopita dhidi ya Burnley kupachika bao la pili na la ushindi kwa Chelsea.
Chelsea pia wataongezwa nguvu baada ya kurudi Wachezaji wao Didier Drogba, Salomon Kalou na Mikel Obi waliokuwa Angola kwenye Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika.
Hull City nao huenda wakamchezesha Mchezaji wao mpya kutoka Misri Amr Zaki ambae alianza kucheza mechi ya juzi akitokea benchi walipocheza na Wolves.
Endapo Chelsea atashinda mechi hii atakuwa amejivuta pointi 4 mbele ya Timu ya Pili Manchester United na Timu zitakuwa zimecheza mechi sawa.
Mechi hii itaanza saa 4 dakika 45 saa za bongo.

No comments:

Powered By Blogger