Friday 5 February 2010

LIGI KUU: Jumamosi Dabi ya Liverpool, Jumapili Bigi Mechi London!!!
• Liverpool v Everton
• Chelsea v Arsenal
Wikiendi hii kuna jumla ya mechi 10 za Ligi Kuu England lakini gumzo kubwa ni mechi mbili nazo ni lile fungua dimba la Jumamosi Dabi ya Jiji la Liverpool huko Uwanja wa Anfield kati ya Wenyeji Liverpool na Mahasimu wao wakubwa Everton mechi itakayo kuwa ya kwanza kuchezwa hapo saa 9 dakika 45 mchana, bongo taimu.
Jumapili ni hekaheka Jijini London, Uwanjani Stamford Bridge, Chelsea wakiwa nyumbani watawaita Arsenal ambao wmetoka freshi tu toka kwenye kipondo cha mabao 3-1 toka kwa Mabingwa Manchester United.
Mpaka sasa takwimu muhimu za LIGI KUU ni:
MSIMAMO LIGI KUU England:
[Timu zimecheza mechi 24 isipokuwa inapotajwa]
1 Chelsea pointi 55
2 Man Utd pointi 53
3 Arsenal pointi 49
4 Tottenham pointi 42
5 Liverpool pointi 41
6 Manchester City pointi 41 [mechi 22]
7 Aston Villa pointi 40 [mechi 23]
8 Birmingham pointi 34 [mechi 23]
9 Everton pointi 32 [mechi 23]
10 Fulham pointi 30
11 Blackburn pointi 28
12 Stoke pointi 26 [mechi 26]
13 Sunderland pointi 24 [mechi 23]
14 Wigan pointi 22 [mechi 22]
15 West Ham pointi 21 [mechi 23]
16 Bolton pointi 21 [mechi 22]
17 Wolves pointi 21 [mechi 23]
18 Hull pointi 21
19 Burnley pointi 20 [mechi 23]
20 Portsmouth pointi 15 [mechi 23]
WAFUNGAJI BORA:
1 Wayne Rooney 20
2 Jermaine Defoe 15
   Didier Drogba 15
3 Darren Bent 14
4 Carlos Tevez 12
   Fernando Torres 12
   Carlos Tevez 12
5 Louis Saha 11
   Cesc Fabregas 11
6 Gabriel Agbonlahor 10
   Frank Lampard 10
Mancini alia kutompata Mkenya Mariga!!!
Bosi wa Manchester City Roberto Mancini ameuita uamuzi wa kutompa kibali cha kazi Mchezaji kutoka Kenya McDonald Mariga [pichani] na hivyo kumkosesha kuwa Mchezaji wa Klabu yake katika siku ya mwisho ya uhamisho ni wa ‘kuwashangaza mno!’
Mariga ambae alianza kucheza Ulaya huko Sweden na Klabu ya Helsingborgs na kisha kwenda Italia Klabu ya Parma alinyimwa kibali cha kazi kwa kuwa tu Kenya haimo kwenye Nchi 70 bora duniani katika listi ya FIFA.
Mancini amelalama: “Tulikuwa tunawawinda Wachezaji kama watatu hivi lakini Mariga alikuwa ndie chaguo letu la kwanza! Inashangaza, Mariga ni Kijana mzuri tu aliecheza Sweden na Italia kwa miaka 6 sasa na uhusiano wa Kiinchi kati ya Uingereza na Kenya ni mzuri! Sielewi kwanini wamekataa kumpa kibali!”
Inasemekana ishu ya Mariga iliingiliwa kati na hata Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga ili kuokoa jahazi dakika za mwisho kwa kuongea na wazito wenzake huko Uingereza lakini hilo halikufua dafu na uhamisho ulishindikana hadi dirisha la uhamisho kufungwa.
Sasa Mariga amehamia kwa Jose Mourinho Klabu ya Inter Milan.

No comments:

Powered By Blogger