Friday 5 February 2010

MENEJA WA POMPEY DANGURONI: Mke amtetea kazi ngumu humfanya ahitaji kukandwa!!!
Mke wa Avram Grant, Meneja wa Portsmouth aliekutwa anatoka kwenye danguro, amemtetea Mumewe kwa kudai anahitaji kukandwa na kuchuliwa kwa sababu anafanya kazi ngumu mno ya kuiongoza Portsmouth ambayo ni Timu uchwara.
Mke huyo wa Grant, aitwae Tzofit Grant ni Mtangazaji wa TV maarufu na mwenye vituko huko kwao Israel, amesisitiza kuwa hajakasirika kwa Mume wake kwenda kukandwa na akaongeza kuwa yuko huru kufanya anachotaka kwa mwili wake.
Bibi huyo aliongeza kuwa ni yeye ndie anaemsistiza kwenda kukandwa na kuchuliwa.
Mama Grant, mwenye umri wa miaka 45, amesema: “Sielewi kwa nini habari hizi zimeleta msisimko. Avram anapenda kukandwa! Mie sijakasirika! Yeye ni Meneja wa Portsmouth. Hivi mnajua kazi hiyo ilivyo ngumu? Yeye ni Meneja mzuri sana kwenye Timu uchwara! Anafanya kazi ngumu sana, anahitaji kukandwa mara mbili kwa siku na tena toka kwa Wanawake wawili na si mmoja!”
Portsmouth wako mkiani kwenye Ligi Kuu na wana matatizo makubwa kifedha yaliyosababisha Klabu hiyo kubadilisha Wamiliki wanne katika msimu huu na pia Wachezaji kucheleweshewa Mishahara yao.
Mke huyo wa Grant ambae husifika kwa vituko vya ajabu kwenye kipindi chake cha TV kikiwemo kunywa mkojo wake kwenye programu laivu na kukoga chokoleti ya majimaji aliongeza na kusema Mumewe alimpigia simu na kumwambia sasa jina lake limetajwa kwamba kaenda danguro na yeye akacheka sana.
Mama huyo akahoji: “Yeye alikwenda kukandwa. Hakuna mtu aliethibitisha hapo ni danguro. Hebu tuwe wakweli, nani anaweza kwenda danguroni mchana kweupe huku kavaa magwanda ya Timu ya Portsmouth wakati akijijua yeye ni mtu maarufu?”
Klabu ya Portsmouth imethibitisha kuwa hawana ishu na Grant kuhusu matembezi hayo kwenye danguro kwani suala hilo haliingiliani na kazi yake.

No comments:

Powered By Blogger