Friday 5 February 2010

Mahakama yaifutia Chelsea adhabu ya kutosajili Wachezaji!!
Mahakama ya Usuluhishi katika Michezo [CAS=Court of Arbitration for Sports] imeondoa kizuizi kilichowekwa na FIFA kwa Chelsea kutosajili Wachezaji hadi mwaka 2011 kufuatia kupatikana na hatia ya kumrubuni na kumchukua Mchezaji chipukizi Gael Kakuta kutoka Klabu ya Ufaransa Lens mwaka 2007 kinyume cha taratibu.
Mwaka jana, FIFA iliifungia Chelsea kutosajili kwa vipindi viwili vya usajili pamoja na kuitaka iilipe fidia Lens.
Gael Kakuta alifungiwa miezi minne na kutakiwa kuilipa Lens kwa kumgharamia.
Chelsea ikakata rufaa CAS na hivyo adhabu zake zikasimama hadi uamuzi wa Mahakama hiyo ulipotakiwa kutolewa na hili lilimruhusu Gael Kakuta kuichezea mechi moja Chelsea kwenye Ligi Kuu mwezi Novemba dhidi ya Wolves.
CAS imeondoa adhabu kwa Chelsea baada ya Klabu hizo mbili, Chelsea na Lens, kufikia makubaliano nje ya Mahakama ambayo inasadikiwa ni pamoja na Chelsea kuilipa fedha Lens.
Uamuzi huu unamaanisha kuwa Chelsea wako huru kusajili Wachezaji dirisha la uhamisho litakapofunguliwa mwishoni mwa msimu huu mwezi Juni.

No comments:

Powered By Blogger