Saturday 6 February 2010

Man United kidedea, ipo kileleni!!
Manchester United wakiwa nyumbani Old Trafford leo wameitandika Timu iliyo mkiani Portsmouth kwa mabao 5-0 na kuchukua uongozi wa Ligi Kuu kutoka kwa Chelsea ambao kesho wana kibarua mahsusi watakapoivaa Arsenal huko Stamford Bridge.
Ili kutwaa tena uongozi wa Ligi kesho lazima Chelsea aifunge Arsenal kwani Manchester United sasa ana pointi 56 na tofauti ya magoli ni 41 na Chelsea ana pointi 55 na tofauti yao ya magoli ni 38 na hivyo akitoka sare na Arsenal, Chelsea atakuwa pointi sawa na Man United lakini Manu United watakuwa juu kwa ubora wao wa tofauti ya magoli.
Arsenal ni watatu na wana pointi 49.
Katika kisago hicho cha Old Trafford, Wayne Rooney ndie aliefungua mafuriko pale alipofunga bao dakika ya 40 kufuatia kona fupi ya Nani kumpa Fletcher alietia majalo tamu na Rooney akamaliza kwa kichwa.
Dakika 1 kabla ya mapumziko kizaazaa cha Nani kikazalisha bao la pili baada ya Beki Vanden Borre kujifunga mwenyewe.
Kipindi cha pili bao zikaongezwa kupitia Michael Carrick ambae kigongo chake kilimbabatiza Hughes wa Portsmouth na kutinga. Berbatov akapachika bao la 4 baada ya kuonyesha utaalam wa hali ya juu na bao la 5 Portsmouth walijifunga wenyewe baada ya krosi kuingizwa wavuni na Beki Wilson.
Vikosi vilivyoanza:
Man Utd: Van der Sar, Neville, Brown, Jonathan Evans, Evra, Valencia, Carrick, Fletcher, Nani, Berbatov, Rooney.
Akiba: Kuszczak, Owen, Park, Fabio Da Silva, Gibson, De Laet, Diouf.
Portsmouth: James, Vanden Borre, Rocha, Wilson, Ben-Haim, Webber, Hughes, Mullins, O'Hara, Belhadj, Piquionne.
Akiba: Ashdown, Owusu-Abeyie, Finnan, Boateng, Dindane, Yebda, Basinas.
Refa: Lee Mason
MATOKEO MECHI ZA Jumamosi, Februari 6
Liverpool 1 v Everton 0
Bolton 0 v Fulham 0
Burnley 2 v West Ham 1
Hull 2 v Man City 1
Man Utd 5 v Portsmouth 0
Stoke 3 v Blackburn 0
Sunderland 1 v Wigan 1
[MECHI INAANZA saa 2 na nusu usiku saa za bongo]
Tottenham v Aston Villa

No comments:

Powered By Blogger