Tuesday 13 April 2010

Adebayor astaafu Togo
Nahodha wa Timu ya Taifa ya Togo, Emmanuel Adebayor, anaechezea Manchester City, ametangaza rasmi kustaafu kuichezea Nchi yake Togo.
Timu ya Togo ilipata maafa Januari 8 iliposhambuliwa kwa risasi ikiwa kwenye Basi wakitokea Congo na kuingia Jimbo la Cabinda, Angola kwenda kushiriki Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika na Dereva wa Basi hilo pamoja na Maafisa wawili wa Togo wakauawa.
Togo ilijitoa Mashindanoni na baadae CAF ikaifungia Miaka minne.
Adebayor ametaja maafa hayo kuwa ndio yaliyochangia kwenye uamuzi wake.
Chelsea kuchanja mbuga?
Leo usiku, Chelsea wana nafasi ya kuongeza tofauti ya pointi kati yao na Manchester United, walio nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu, kufikia pointi 4 watakapoikaribisha Bolton Wanderers Stamford Bridge.
Juzi, Man United walishindwa kuipiku Chelsea walipotoka sare 0-0 na Blackburn na hilo limemfanya Sir Alex Ferguson kukiri Ubingwa ni mgumu kwao na pia kusema mechi ya leo ni ubwete kwa Chelsea kauli iliyochekwa na Meneja wa Bolton, Owen Coyle, aliesema wao lengo lao ni kugangamara.
Van Persie kurudi Jumatano?
Arsenal Jumatano wapo kwenye dabi ya Timu za London ya Kaskazini watakaposafiri kwenda White Hart Lane kuivaa Tottenham katika mechi ya Ligi Kuu na hiyo ni mechi muhimu kwao kwani ushindi utaifanya waichomoe Manchester United toka nafasi ya pili lakini kwa Washabiki wa Ze Gunners kumuona Straika wao mahiri Robin van Persie akiwa Uwanjani ndio kutaleta furaha kubwa.
Van Persie yuko nje ya Uwanja tangu Novemba alipoumia enka akichezea Nchi yake Uholanzi mechi ya kirafiki na Italia.

No comments:

Powered By Blogger