Sunday 11 April 2010

EL CLASICO: Real 0 Barca 2
FC Barcelona jana waliifunga Real Madrid bao 2-0 katika BIGI MECHI ya huko Spainiliyofanyika nyumbani kwa Real Uwanja wa Santiago Bernabeau na kushuhudiwa na Mamilioni kila kona ya Dunia.
Barcelona sasa wamekamilisha vipigo viwili kwa Real kwenye La Liga baada ya kushinda mechi ya kwanza kati yao bao 1-0 mwezi Novemba na ushindi wa jana umewapa uongozo wa Ligi wakiwa pointi 3 juu ya Real huku zimebaki mechi 7.
Ni yule Mchawi Duniani Lionel Messi alieipatia Barca bao la kwanza ya dakika ya 33 baada ya kumtoka Beki Raul Albiol na kumhadaa Kipa Iker Casillas.
Pedro aliipatia Barca bao la pili dakika ya 56 kufuatia bonge la pande kutoka kwa Xavi.

No comments:

Powered By Blogger