Wednesday 14 April 2010

Chelsea haooo..............!!!!!!
Chelsea 1 Bolton 0
Chelsea wamechanja mbuga na wako pointi 4 mbele katika uongozi wa Ligi kukiwa kumebaki mechi 4 Ligi kwisha baada ya kuitungua Bolton Wanderers bao 1-0.
Wakicheza kwao Stamford Bridge, Chelsea hawakuonekana kuwa kwenye fomu lakini Nicolas Anelka aliwapa ushindi dakika tatu kabla ya haftaimu alipofunga kwa kichwa baada ya krosi ya Didier Drogba.
Chelsea sasa wana pointi 77, Man United 73 na Arsenal 71 lakini leo wapo White Hart Lane kuikwaa Tottenham na ushindi kwao utawafanya wachupe nafasi ya 2.
Mechi za leo ni:
Jumatano, 14 Aprili 2010
[saa 3 dak 45 usiku]
Aston Villa v Everton
Wigan v Portsmouth
[saa 4 usiku]
Tottenham v Arsenal

No comments:

Powered By Blogger