Sunday 11 April 2010

LIGI KUU: Wolves 0 Stoke 0
Hii ndio mechi ya kwanza ya Ligi Kuu kuchezwa leo Jumapili na ilimalizika kwa sare ya 0-0 huku Watazamaji wakipiga kelele kuikejeli mechi yenyewe kwa kupiga mbiu: “Imepooza! Imepooza!”.
Lakini hilo si ajabu kwani Stoke tayari wako salama kushushwa Daraja na Wolves leo wamejihakikishia kuwa pointi 6 juu ya zile Timu 3 zilizo mkiani ambazo ndizo ziko hatarini kushushwa Daraja huku zimebaki mechi 4 tu.
O’Neill amponda Refa Webb
Msimu huu, kila baada ya mechi imekuwa kawaida kwa Mabosi wa Timu kulalamikia uamuzi na Nusu Fainali ya FA Cup ya jana ambayo Chelsea walitandika Aston Villa bao 3-0, haikuwa tofauti.
Bosi wa Aston Vlla, Martin O’Neill amelia na Refa Howard Webb, ambae ni mmoja wa Marefa watakaochezesha Kombe la Dunia huko Afrika Kusini kuanzia Juni 11, kuhusu matukio mawili ya mechi hiyo jana.
O’Neill amefoka: “Sijui kama uliiona ile rafu ya Terry kwa Milner! Ni mbaya! Milner ana bahati kubwa hakuvunjwa! Ile ni Kadi Nyekundu! Na Refa alikuwa hapo hapo!”
Tukio la pili ni pale Mikel John Obi alipomchezea rafu Gabriel Agbonlahor ndani ya boksi na Refa Webb kupeta.

No comments:

Powered By Blogger