Sunday 11 April 2010

Liverpool nao.........................…kisikiiiiiii!
Liverpool wametoka sare ya 0-0 Uwanjani kwao Anfield walipocheza na Fulham kwenye mechi ya Ligi Kuu na inaelekea ile nafasi ya 4 kwao inaanza kuota mbawa kwani wapo nafasi ya 6 na wamebakisha mechi 4 na juu yao zipo Tottenham na Manchester City ambazo licha ya kuwa na pointi zaidi ya Liverpool pia wana mechi mkononi.
Liverpool wamecheza mechi 34 na wana pointi 56, Tottenham mechi 32 pointi 58 na Man City ndio wako nafasi ya 4 kwa mechi 32 na pointi 59.
Leo Liverpool ilicheza bila ya Staa Fernando Torres na pengo lake lilionekana kwani licha ya kutawala walishindwa kufunga.
Vikosi vilivyoanza:
Liverpool: Reina, Johnson, Kyrgiakos, Carragher, Agger, Aquilani, Mascherano, Maxi, Gerrard, Babel, Ngog.
Akiba: Cavalieri, Benayoun, Kuyt, Lucas, Degen, Ayala, Pacheco.
Fulham: Schwarzer, Baird, Hangeland, Hughes, Konchesky, Greening, Murphy, Etuhu, Duff, Nevland, Zamora.
Akiba: Zuberbuhler, Kelly, Shorey, Okaka, Riise, Smalling, Dikgacoi.
Refa: Andre Marriner

No comments:

Powered By Blogger