Sunday 11 April 2010

AS Roma yaishusha Inter kileleni
Kwa mara ya kwanza katika Miezi mitano, Inter Milan imepokonywa uongozi wa Serie A na AS Roma walioshinda 2-1 leo dhidi ya Atalanta.
Jana Timu ya Jose Mourinho, Inter Milan, ilitoka sare 2-2 na Fiorentina.
Mabao ya AS Roma, inayoongozwa na Meneja Claudio Ranieri, yalifungwa na Mirko Vucinic na Marko Cassetti.
AS Roma sasa wana pointi 68 na Inter wapo pointi moja nyuma huku zikiwa zimebaki mechi 5.
Nafasi ya 3 imeshikwa na AC Milan ambao walitoka sare na Catania ya bao 2-2 na sasa wako pointi 4 nyuma ya Inter.

No comments:

Powered By Blogger