Thursday 15 April 2010

Barca yaisuta Arsenal
Barcelona wamegoma kuwa wana makubaliano na Arsenal ya kutomrubuni Cesc Fabregas na hilo linapingana na kauli ya Mwenyekiti wa Arsenal, Peter Hill-Wood, ambae alitamka kuwa wana makubaliano na Barcelona ya kuitaka Klabu hiyo ya Spain isimrubuni Nahodha Wao Cesc Fabregas ambae amekuwa akivumishwa kwa muda mrefu kuwa yuko njiani kwenda Barcelona Msimu ujao.
Hill-Wood alisema: “Tuna makubaliano na Barca ya kuwataka wasimfuate Fabregas ila baadae wanaweza kuja kwetu moja kwa moja."
Lakini Katibu wa Ufundi wa Barcelona Txiki Begiristain amesisitiza hawana makubaliano yeyote na Arsenal na kama wakimtaka Fabregas wataongea na Arsenal.
Begiristain amesema: ‘Hatujasema hatutamsaini. Tukimtaka tutaanzisha mazungumzo!”
PFA yatoa Listi ya Wagombea Mchezaji Bora wa Mwaka
Straika wa Manchester United na England, Wayne Rooney, yumo katika Listi ya Wagombea wanne na ndie anaepewa nafasi kubwa ya kushinda Tuzo ya Mchezaji Bora ya PFA [Chama cha Wachezaji wa Kulipwa wa Soka].
Wengine kwenye Listi hiyo ni Kiungo wa Arsenal Cesc Fabregas, Didier Drogba wa Chelsea na Carlos Tevez wa Manchester City.
Rooney na Fabregas pia wamo kwenye Listi kama hiyo lakini ya Vijana na wanaungana na James Milner wa Aston Villa na Kipa wa Birmingham Joe Hart kwenye Listi hiyo.
Ikiwa Rooney atashinda Tuzo hiyo hii itakuwa ni mara ya 4 mfululizo kwa Mchezaji wa Manchester United kuinyakua.
Wachezaji wengine wa Man United walioshinda Tuzo hiyo ni Cristiano Ronaldo alieshinda mwaka 2007 na 2008 na mwaka jana Ryan Giggs ndie alieinyakua.
Rooney na Fabregas washawahi kushinda Tuzo hii kwa Vijana hapo nyuma wakati Rooney alipoinyakua mwaka 2005 na 2006 na Fabregas kushinda 2008.

No comments:

Powered By Blogger