Sunday 11 April 2010

Man United wakwaa kisiki, Chelsea wachekelea!!
Wakiwa ugenini Ewood Park, Manchester United leo wamewapa nafuu kubwa Wapinzani wao wakubwa katika kinyang’anyiro cha kutwaa Ubingwa Msimu huu, Chelsea, walipotoka sare ya 0-0 na Blackburn Rovers.
Kwa matokeo hayo, Chelsea bado wapo kileleni wakiwa na pointi 74 na Man United ni wa pili wakiwa na pointi 73 lakini sasa wamecheza mechi moja zaidi ya Chelsea.
Mechi inayofuata kwa Chelsea ni Jumanne watakapokuwa kwao Stamford Bridge kucheza na Bolton Wanderers.
Vikosi vilivyoanza:
Blackburn: Robinson, Salgado, Samba, Jones, Givet, Nzonzi, Grella, Emerton, Pedersen, Olsson, Kalinic.
Akiba: Brown, Nelsen, Dunn, Roberts, Andrews, Diouf, Di Santo.
Man Utd: Van der Sar, Neville, Ferdinand, Vidic, O'Shea, Valencia, Scholes, Giggs, Nani, Berbatov, Macheda.
Akiba: Kuszczak, Evra, Park, Jonathan Evans, Fletcher, Obertan, Gibson.
Refa: Peter Walton

No comments:

Powered By Blogger