Wednesday 14 April 2010

Bolton wadai Chelsea wanabebwa!!!
Meneja wa Bolton Owen Coyle amemlaumu Refa Lee Probert kwa kuwanyima penalti mbili katika mechi ya jana ya Ligi Kuu ambayo Chelsea waliifunga Bolton 1-0 Uwanjani Stamford Bridge na kujichimbia uongozi wa Ligi wakiwa pointi 4 mbele.
Coyle amedai Drogba aliunawa mpira kipindi cha kwanza na John Terry nae aliucheza mpira kwa mkono kipindi cha pili na zote zilikuwa ni penalti za wazi.
Coyle amelalamika: “Hatukuhitaji bahati leo, tulihitaji Marefa waamue kwa haki!”
Coyle amedai Msaidizi wa Refa alisema ttukio la Terry mpira ulimgonga begani lakini Coyle amesisitiza alicheza wazi wazi kwa mkono.

No comments:

Powered By Blogger