Sunday 11 April 2010

Mechi zao ni 0-0, nini walisema………:
==Bosi wa Liverpool Rafael Benitez: "Nimesikitishwa. Nafasi ya 4 sasa iko mbali. Inategemea Timu nyingine, Timu 2 au 3 zitusaidie. Hilo ni kubwa mno. Torres hakucheza ameenda kuonana na Daktari Bingwa.”
==Meneja Msaidizi Man United Mike Phelan: "Sasa unaanza kuangalia matokeo ya Timu nyingine! Hatukubahatika leo lakini hata uteuzi wetu wa Timu haukuwa mzuri! Hatuwezi kumtegemea Rooney tu ingawa ni Mchezaji wetu mzuri! Hii ni Manchester United na Wachezaji wengine wanatakiwa waonyeshe kwa nini Klabu hii iliwanunua!”
==Bosi wa Blackburn Sam Allardyce: "Tulicheza jihadi na kupata pointi moja ni manufaa kwetu! Najua tunashindwa kufunga Msimu huu lakini defensi yetu ni nzuri!”
Man City yaishindilia Birmigham na kujichimbia nafasi ya 4
Wakiwa kwao City of Manchester Stadium, Manchester City leo wameitandika Birmingham mabao 5-1 na kutuma salam kwa Tottenham na Liverpool kuwa nafasi ya 4 kwenye Ligi Kuu ni yao.
Man City waliandika bao la kwanza kwa penalti iliyotolewa na Refa Phil Dowd dakika ya 35 pale Adebayor alipoingia ndani ya boksi na kuangushwa na Scott Dann.
Tevez akapiga penalti hiyo na kufunga bao la kwanza.
Dakika 5 baadae Man City wakawa bao 2 mbele kufuatia kona ya Adam Johnson kumkuta Nedum Onuoha aliefunga kwa kichwa.
Dakika 2 baadae Birmingham wakapata bao kupitia Cameron Jerome alieunganisha kwa kichwa krosi ya James McFadden.
Kabla ya mapumziko, Man City wakapachika bao la 3 baada ya mpira mrefu kukimbiliwa na Craig Bellamy alieuwahi kabla ya Kipa Maik Taylor na kumpasia Adebayor aliefunga kilaini.
Kipindi cha pili, Nedum Onuoha akafunga bao la 4 kwa Man City kwa mkaju toka nje ya boksi.
Katika dakika za lala salama, Adebayor akapachika bao la 5 na kuweza kuuchukua mpira uliochezewa mechi hii kuwa mali yake kwa vile amefunga bao 3 katika hii mechi.
Vikosi vilivyoanza:
Man City: Given, Onuoha, Kompany, Toure, Garrido, Adam Johnson, Vieira, Barry, Bellamy, Tevez, Adebayor.
Akiba: Nielsen, Wright-Phillips, Santa Cruz, De Jong, Boyata, Cunningham, Ibrahim.
Birmingham: Taylor, Carr, Johnson, Dann, Ridgewell, Gardner, Bowyer, Ferguson, Fahey, Jerome, McFadden.
Akiba: Doyle, Larsson, Phillips, Benitez, Michel, Parnaby, Vignal.
Refa: Phil Dowd

No comments:

Powered By Blogger