Thursday 15 April 2010

Wenger Mikono juu Ubingwa!!
Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, amesema Timu yake iusahau Ubingwa kufuatia kichapo cha Jumatano cha 2-1 mikononi mwa Tottenham kilichowafanya wawe pointi 6 nyuma ya vinara Chelsea na mechi zikiwa zimebaki 4.
Wenger amesema: “Ubingwa basi! Sisi tufikirie kumaliza juu kadri tuwezavyo!”
Wenger amekiri Timu yake haijakomaa na hilo limeonekana walipofungwa na Tottenham kwani mechi hizo ndizo za kushinda ili kuonyesha umekomaa.
Hata hivyo, Wenger amesisitiza wao wataendelea kupigana hadi mwisho ingawa sasa nafasi yao ya Ubingwa ni finyu.
Pia, Wenger alionyesha kufurahishwa na kurudi Uwanjani kwa Straika wake mahiri Robin van Persie alieingizwa mwishoni baada ya kupona enka iliyomweka miezi mitano nje.
Wenger alisema alipoingia Van Persie Arsenal ilibadilika na kuwa na uhai mbele.

No comments:

Powered By Blogger