Saturday 17 April 2010

Ni siku njema kwa Man United!!!
Chelsea yashindiliwa, Man United wawaliza Mahasimu sekunde ya mwisho!!
Katika dabi ya Manchester iliyochezwa City of Manchester Stadium, Manchester United waliwatungua Mahasimu wao wakubwa Manchester City kwa bao 1-0 bao lililofungwa na Paul Scholes katika sekunde za mwisho za gemu hiyo.
Katika mechi iliyofuata baadae, wamepata pigo kubwa walipowashwa na Tottenham bao 2-1 Uwanjani White Hart Lane na kufanya wawe pointi moja tu mbele ya Man United huku kukiwa kumebaki mechi 3.
Ushindi wa Tottenham umewafanya washikilia nafasi ya 4 na sasa wana pointi 64 na Man City wako nafasi ya 5 wakiwa na pointi 62.
Mabao ya Tottenham yalifungwa na Jermaine Defoe kwa penalti na Bale akafunga bao la pili.
Hakika ni siku tamu kwa Man United kwa matumaini yao ya kutwaa Ubingwa tena kufufuliwa tena.
MATOKEO KAMILI MECHI ZA LEO:
Birmingahm 0 Hull City 0
Blackburn 2 Everton 3
Fulham 0 Wolves 0
Man City 0 Man United 1
Stoke 1 Bolton 2
Sunderland 2 Burnley 1
Tottenham 2 Chelsea 1

No comments:

Powered By Blogger