Friday 16 April 2010

Mancini apatikana na hatia, akwepa kifungo,apigwa Faini
Bosi wa Manchester City Roberto Mancini amepatikani na hatia kwa kosa la kutokuwa na mwenendo mzuri na hivyo kupigwa Faini ya Pauni Elfu 20 na FA kufuatia mshikemshike kati yake na Meneja wa Everton, David Moyes, uliotokea Machi 24 Man City ilipoikaribisha Everton City of Manchester Stadium na Refa wa mechi hiyo akalazimika kuwatoa wote wawili Uwanjani.
Mancini alikiri kosa lake na akaomba adhabu ndogo kwa vile ni kosa lake la kwanza na pia alikwisha kumuomba msamaha David Moyes mara baada ya mechi hiyo.
Faini ya Mancini imesitishwa hadi mwishoni mwa Msimu wa 2011/12 ili kumwangalia asifanye kosa hadi wakati huo.

No comments:

Powered By Blogger