Monday 12 April 2010

Ubingwa ni utata - Ferguson
Bosi wa Manchester United Sir Alex Ferguson amekiri kuchukua Ubingwa ni mzigo mkubwa kwao kufuatia sare yao ya 0-0 na Blackburn Jumapili.
Man United walikosa nafasi kadhaa za kufunga katika mechi hiyo na Ferguson amekiri: “Ni pigo, hamna ubishi! Sasa ni ngumu sisi kuchukua Ubingwa! Ni matokeo mazuri kwa Chelsea!”
Chelsea bado ni vinara na wana pointi 74 na Man United ni wa pili wana pointi 73 lakini wamecheza mechi moja zaidi ya Chelsea.
Wakicheza bila ya Mfungaji wao mkuu, Wayne Rooney, Ferguson aliwachezesha Chipukizi Frederico Macheda na Dimitar Berbatov kama Mastraika lakini Macheda alipwaya na kutolewa dakika ya 65 na kuingizwa Ji-Sung Park.
Nae Berbatov, huku zikiwa zimebaki dakika 10 mechi kwisha, alikosa bao la wazi.
Lakini ni makosa ya Winga Valencia ya kipindi cha kwanza ndio Ferguson aliyazungumzia pale Valencia alipokosa bao la wazi akiwa uso kwa uso na Kipa Robinson na kumpelekea mpira moja kwa moja badala ya kupiga pembeni.
Mechi inayofuata kwa Man United ni ile dabi yao na Mahasimu wao Manchester City siku ya Jumamosi Uwanja wa City of Manchester.
Chelsea wao wanacheza Jumanne na Bolton na Jumamosi wana dabi ya Timu za London watakapocheza na Tottenham.

No comments:

Powered By Blogger