Saturday 10 April 2010

FA Cup: Chelsea wako Fainali!!
• Chelsea 3 Villa 0
Chelsea leo wametinga Fainali ya Kombe la FA walipoichapa Aston Villa bao 3-0 na bao zote zilifungwa kipindi cha pili.
Fainali hiyo itafanyika Uwanja wa Wembley Mei 15 na Chelsea watakutana na Mshindi wa mechi ya kesho kati ya Tottenham na Portsmouth.
Villa walitawala mechi hii kipindi cha kwanza na ilionekana wazi Refa Webb amewanyima penalti ya wazi kwenye dakika ya 17 pale Mikel Obi alipomwangusha Agbonlahor ndani ya boksi.
Kipindi cha pili Chelsea walibadilika na kutawala na kona yao ya dakika ya 67 iliokolewa kizembe na Villa na kumkuta John Terry alieupiga mpira golini na kumfikia Didier Drogba aliefunga.
Dakika ya 89, krosi nzuri toka wingi ya kulia ya Michael Ballack ilimpata Malouda aliemalizia na kufunga.
Chelsea walipata bao la 3 dakika za majeruhi Mfungaji akiwa Frank Lampard kufuatia kaunta ataki iliyowahusisha Malouda na Anelka aliemsogezea Lampard.
Vikosi vilivyoanza:
Aston Villa: Friedel, Cuellar, Dunne, Collins, Warnock, Ashley Young, Milner, Petrov, Downing, Agbonlahor, Carew.
Akiba: Guzan, Luke Young, Sidwell, Delfouneso, Delph, Heskey, Beye.
Chelsea: Cech, Paulo Ferreira, Terry, Alex, Zhirkov, Deco, Mikel, Lampard, Joe Cole, Drogba, Malouda.
Akiba: Hilario, Ivanovic, Ballack, Kalou, Sturridge, Belletti, Anelka.
Refa: Howard Webb

1 comment:

Anonymous said...

KAKA GOLI LA PILI SI DKK YA 67. THEN NAONA LEO UMEKUWA FASTA KUPOSTI MATOKEO, ILA MAN IKIFUNGWA NA BLOG INAPOTA KWIKWIIIZ. KAAAZ KWELIKWELI

Powered By Blogger