Tuesday 6 April 2010

Mourinho auita Uwanja wa Luzhniki wa kitoto!
Kocha wa Inter Milan, Jose Mourinho, ambae leo yuko Moscow na Timu yake kurudiana na CSKA Moscow katika mechi ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI kwenye Uwanja wa Luzhniki ambao nyasi zake ni za bandia, ameuita Uwanja huo ni wa kitoto.
Inter Milan, walioshinda mechi ya kwanza kwa bao 1-0, leo wanahitaji suluhu tu iliwatinge Nusu Fainali kucheza na Mshindi wa mechi nyingine ya leo kati ya Barcelona na Arsenal.
Mourinho amesema alitaniana na Wachezaji wake kwa kuwaambia walipokuwa Watoto walicheza mpira barabarani hivyo leo hawawezi kushindwa kucheza kwenye Uwanja wenye nyasi bandia kwani ni sawa na uwanja wa kitoto.
Timu nyingi zimekuwa zikiulalamikia Uwanja huo wa Luzhniki na wengi wanahisi CSKA Moscow wanafaidika sana kwa kucheza hapo.

No comments:

Powered By Blogger