Friday 9 April 2010

Baada ya kupondwa UEFA CHAMPIONS LIGI, England ina Timu 2 Nusu Fainali EUROPA LIGI!!!
• Ni Liverpool v Athletico Madrid na Fulham v Hamburg!!
Wolfsburg 0 Fulham 0
Ile mbiu ya kutaka Bobby Zamora achukuliwe Kikosi cha England cha Kombe la Dunia jana iliendelea kupata nguvu zaidi pale Straika huyo ambae sasa yupo kwenye fomu ya hali ya juu alipofunga bao la ushindi sekunde ya 21 tu ya mchezo na kuifikisha Timu iliyokuwa haitegemewi na wengi Nusu Fainali ya EUROPA LIGI ambako watacheza na Hamburg ambao jana waliwatupa nje Standard Lege walipowakung’uta bao 3-1.
Wakiwa ugenini Ujerumani,Bobby Zamora alimzunguka Beki Simunek na kwa utulivu na ufundi mkuu alipachika bao kwenye sekunde ya 21 tangu maechi ianze na kuifanya Fulham isonge mbele kwa jumla ya bao 3-1 baada ya kushinda nyumbani bao 2-1.
Vikosi vilivyoanza:
Wolfsburg: Benaglio, Pekarik, Simunek, Barzagli, Schafer, Riether, Josue, Gentner, Misimovic, Grafite, Dzeko.
Akiba: Lenz, Martins, Hasebe, Johnson, Dejagah, Schindzielorz, Rever.
Fulham: Schwarzer, Baird, Hughes, Hangeland, Konchesky, Murphy, Etuhu, Duff, Gera, Davies, Zamora.
Akiba: Zuberbuhler, Kelly, Nevland, Riise, Smalling, Greening, Dikgacoi.
Refa: Viktor Kassai (Hungary)
Liverpool 4 Benfica 1
Liverpool jana waliendelea kujipa matumaini ya angalau kubeba Kombe moja Msimu huu pale walipokipindua kipigo cha 2-1 katika mechi ya kwanza na kuiwasha Benfica bao 4-1 na hivyo kutinga Nusu Fainali ya EUROPA LIGI na watacheza na Atletico Madrid ambao jana waliwabwaga Wahispania wenzao Valencia.
Dirk Kuyt ndie aliefungua kitabu cha magoli pale alipofunga goli baada ya kona lakini Mshika Kibendera alilikataa bao hilo kwa kunyoosha kibendera na ndipo Refa Bjorn Kuipers alipompiku na kulikubali.
Lucas akaongeza bao la pili na Fernando Torres akapiga bao la3.
Benfica wakapata bao moja kufuatia frikiki ya Oscar Cardozo lakini ni Torres tena aliwakata maini na kufunga bao la 4.
Vikosi vilivyoanza:
Liverpool: Reina, Johnson, Carragher, Kyrgiakos, Agger, Mascherano, Lucas, Kuyt, Gerrard, Benayoun, Torres.
Akiba: Cavalieri, Aquilani, Ngog, Degen, El Zhar, Ayala, Pacheco.
Benfica: Julio Cesar, Ruben Amorim, Luisao, Sidnei, David Luiz, Javi Garcia, Carlos Martins, Ramires, Aimar, Di Maria, Cardozo.
Akiba: Moreira, Airton, Maxi Pereira, Fabio Coentrao, Felipe Menezes, Alan Kardec, Eder Luis.
Refa: Bjorn Kuipers (Holland)
MATOKEO KAMILI:
ROBO FAINALI:
Alhamisi, Aprili 8
Atletico Madrid 0 v Valencia 0 [Jumla 2-2, Athletico wanasonga kwa bao za ugenini]
Liverpool 4 v Benfica 1 [5-3]
Standard Liege 1 v Hamburg 3 [2-5]
Wolfsburg 0 v Fulham 1 [1-3]
NUSU FAINALI
Alhamisi, Aprili 22
Hamburg v Fulham
Atletico Madrid v Liverpool
Alhamisi, Aprili 29
Fulham v Hamburg
Liverpool v Atletico Madrid
FAINALI
Jumatano, Mei 12

1 comment:

Anonymous said...

BWAWA LA MAINI NA FULHAM WAING'ARISHA ENGLAND BAADA YA AIBU YA ARSENAL NA MAN U. MAN MMEZOWEA KUBEBWA NDO MAANA HAMWISHI KULALAMIKA. BORA MKICHEZA FG AWE REFA

Powered By Blogger