Sunday 4 April 2010

Burnley 1 Man City 6
Jana katika mechi ya Ligi Kuu iliyochezwa mwishoni, Man City wakiwa ugenini waliichabanga Burnley bao 6-1 na kuchukua nafasi ya 4 inayogombewa na Tottenham, Liverpool na Aston Villa.
Huku mvua kubwa ikinyesha na uwanja kujaa maji, Man City nao walikuwa wakiangusha mvua ya magoli na walikuwa mbele kwa bao 5 wakati wa mapumziko.
Bao za Man City zilifungwa na Adebayor, bao mbili dakika ya 4 na 45, Bellamy dakika ya 5, Tevez dakika ya 7, Vieira dakika ya 20 na Kompany dakika ya 58.
Fletcher ndie aliewafungia Burnley bao lao pekee.
Burnley wako nafasi ya 19 ikiwa ni nafasi moja tu toka mkiani walipo Portsmouth.
Juu ya Burnley wapo Hull City na hizo ndizo Timu 3 zilizo hatarini kuporomoka.
ULE ‘WEHU’ KUMPANGA REFA MIKE DEAN WATIMIA!!
Fergie amponda vibaya Dean na wenzake!!!
Sir Alex Ferguson amewaponda vibaya Waamuzi wa pambano la jana la Ligi Kuu kati ya Manchester United na Chelsea ambalo Chelsea walishinda 2-1 na kuukwaa uongozi wa Ligi.
Didier Drogba alifunga bao la pili huku akiwa waziwazi ofsaidi na Ferguson amelaumu kukubaliwa kwa bao hilo.
Katika mechi hiyo Refa Mike Dean, ambae uteuzi wake kuchezesha mechi hiyo uliitwa ‘wehu’ na Meneja wa Burnley Brian Laws baada ya Refa huyo kuwapa Blackburn penalty feki na hivyo Burnley kufungwa, jana alipeta penalti 3 za wazi, mbili za Man United na moja ya Chelsea, pengine akitaka kufuta makosa yake aliyofanya katika mechi kati ya Burnley na Blackburn.
Ferguson alilalamika: “Kitu ambacho sielewi ni Mshika Kibendera kuwa mbele ya Drogba na hakuna hata mtu aliemziba na haoni ofsaidi! Mechi kubwa kama ile unataka Marefa wenye ubora na hatukuwapata! Ni kazi mbovu kabisaa!”
Tangu wiki yote iliyopita Refa Mike Dean amekuwa akimulikwa sana na Vyombo vya Habari baada ya Straika wa Blackburn Martin Olsson kuungama alijidondosha kusudi kwa vile walijua Refa huyo hutoa penalti kirahisi na penalti hiyo ndio iliyowaua Burnley katika mechi ya Ligi wikiendi iliyopita.
Ushindi huo wa Chelsea umewafanya wawe pointi 2 mbele ya Man United huku mechi 5 zimebaki na Ferguson amesema: “Mechi 5 zimebaki, wako pointi 2 mbele na wana goli 4 bora kupita sisi! Hakika wapo nafasi nzuri! Lakini tutabadilika na tunao uwezo wa kushinda mechi zote 5 lakini pengine hata hilo lisitusaidie!”

No comments:

Powered By Blogger