Sunday 4 April 2010

Liverpool yakwaa kigingi!
Uwanja wa Mtakatifu Andrew umewashinda Liverpool kutoka na ushindi pale walipotoka droo na Wenyeji Birmingham kwa bao 1-1 katika moja ya mechi 3 za Ligi Kuu za leo.
Mabao yote ya mechi hii yalifungwa kipindi cha pili.
Liverpool ndio walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia Nahodha wao Steven Gerrard lakini Birmingham wakasawazisha kwa bao la Liam Ridgewell.
Sare ya leo imefanya Liverpool washike nafasi ya 6 wakiwa wamecheza mechi 33 na kuwa na pointi 55.
Juu ya Liverpool wapo Tottenham waliocheza mechi 32 na wana pointi 58.
Nafasi ile ya ‘dhahabu’ inayogombewa na Timu za Manchester City, Tottenham, Liverpool na Aston Villa, nafasi ya 4, imekamatwa na Man City waliocheza mechi 32 na wana pointi 59.
Vikosi vilivyoanza:
Birmingham: Hart, Carr, Johnson, Dann, Ridgewell, Gardner, Ferguson, Bowyer, Fahey, Jerome, McFadden.
Akiba: Taylor, Larsson, Phillips, Benitez, Michel, Parnaby, Vignal.
Liverpool: Reina, Johnson, Carragher, Kyrgiakos, Insua, Benayoun, Gerrard, Lucas, Maxi, Torres, Kuyt.
Akiba: Cavalieri, Aquilani, Agger, Babel, Mascherano, Ngog, Degen.
Refa: Martin Atkinson
Fulham 2 Wigan 1
Katika mechi nyingine ya Ligi Kuu leo Jumapili, Fulham wakiwa kwao Craven Cottage wamefaulu kutoka nyuma na kushinda bao 2-1 dhidi ya Wigan Timu ambayo inachechemea kujinasua toka hatarini.
Wigan ndio walitangulia kufunga bao dakika ya 32 Mfungaji akiwa Jason Scotland bao lililodumu hadi mapumziko.
Fulham wakasawazisha kipindi cha pili dakika ya 6 ya kipindi hicho Mfungaji akiwa Stefano Okaka.
Bao la ushindi la Fulham lilipatikana kupitia Beki wao Brede Hangeland kufuatia kona ya Damien Duff.
Ushindi huu umeiweka Fulham nafasi ya 12 wakiwa na pointi 41 na Wigan wako nafasi ya 16 wakiwa na pointi 31 zikiwa ni pointi 4 tu juu ya Timu zile zilizo eneo la hatari la kuporomoka Daraja.
Vikosi vilivyoanza:
Fulham: Schwarzer, Davies, Hughes, Hangeland, Konchesky, Duff, Murphy, Etuhu, Dempsey, Gera, Elm.
Akiba: Zuberbuhler, Baird, Shorey, Okaka, Nevland, Smalling, Greening.
Wigan: Kirkland, Melchiot, Bramble, Scharner, Figueroa, McCarthy, Moreno, Diame, N'Zogbia, Rodallega, Scotland.
Akiba: Stojkovic, Gohouri, Amaya, Watson, Moses, Gomez, Sinclair.
Refa: Mark Clattenburg

No comments:

Powered By Blogger