Tuesday 6 April 2010

Timu za England hatarini kutocheza Nusu Fainali UEFA
Leo na kesho ndio hatima ya Timu za England kujua wanaingia Nusu Fainali za UEFA CHAMPIONS LIGI au la wakati leo Arsenal atakapojimwaga ugenini Nou Camp kuivaa Barcelona na kesho Manchester United yuko kwake Old Trafford atakaporudiana na Bayern Munich.
Wakati Arsenal anatafuta ushindi au sare ya zaidi ya bao 2-2 kwa vile mechi ya kwanza walitoka suluhu 2-2 na Barcelona, Manchester United ni lazima washinde kwa vile walifungwa 2-1 huko Ujerumani wiki iliyopita.
Arsenal na Manchester United zikitolewa itakuwa ni mara ya kwanza tangu mwaka 2003 kwa England kukosa Timu kwenye Nusu Fainali za UEFA CHAMPIONS LIGI.

No comments:

Powered By Blogger