Monday 5 April 2010

KUNA NINI LIGI ZA ULAYA!
Bordeaux, Manchester United na Schalke zote zilipokonywa uongozi wa Ligi za Nchi zao kufuatia mechi za wikiendi wakati Lyon, Chelsea na Bayern Munich walipoibuka vinara wa Ligi hizo.
Huko Spain na Italy misimamo ya Ligi imebaki kama ilivyokuwa awali ingawa tumbo joto linazidi kupanda.
Ligi Kuu England: Chelsea washika hatamu
Ushindi wa Chelsea wa 2-1 dhidi ya Manchester United umewapa uongozi wa Ligi hii wakiwa pointi mbili mbele ya Man United huku mechi zimebaki 5.
Katika mechi hizo 5 zilizobaki, kimahesabu mechi ngumu kwa Chelsea ni zile dhidi ya Tottenham na Liverpool.
Timu nyingine iliyonufaika sana kwa mechi za wikiendi ni Manchester City ambayo iliichabanga Burnley bao 6-1 na kutwaa nafasi ya 4 ambayo inaliliwa na Timu kadhaa nyingine ili kucheza UEFA Msimu ujao.
Tatu Bora: Chelsea (pointi 74), Manchester Utd (72), Arsenal (71)
Tatu za mkiani: Hull City (pointi 27), Burnley (24), Portsmouth (14)
Wafungaji Bora: Wayne Rooney (26), Didier Drogba (25), Darren Bent (22)
Ligue 1: Bordeaux inaporomoka
Bordeaux walipigwa 2-1 na Nancy na kunyang’anywa uongozi na kuporomoka hadi nafasi ya 4.
Inaelekea msimu wa Bordeaux umeanza kuingia mkosi kwani ghafla umeanza kuharibika pale walipofungwa 3-1 na Marseille kwenye Fainali ya Kombe la Ligi la Ufaransa na mechi iliyofuata ni mkondo wa kwanza wa Mashindano ya UEFA wakapigwa 3-1 na Lyon kisha juzi kwenye Lique 1 wakapokonywa uongozi wa Ligi hiyo walipofungwa na Nancy bao 2-1.
Lyon ndio wametwaa uongozi baada ya kuifunga Rennes 2-1.
Lakini Ligi ni ngumu hasa kwa vile ni pointi 3 tu inazitenganisha Timu 6 za juu na ni pointi moja tu kwa Timu 5 za juu.
Tatu Bora: Lyon (pointi 57, magoli +19), Montpellier (57, +7), Auxerre (57, +6)
Tatu za mkiani: Boulogne (pointi 24), Le Mans (21), Grenoble (15)
Wafungaji Bora: Mamadou Niang (magoli 15), Kevin Gameiro, Lisandro Lopez, Nene and Asamoah Gyan (wote 13 kila mmoja), Gervinho and Mevlut Erdinc (both 12)
Bundesliga: Bayern kileleni
Wakiongozwa na Ribery, Bayern Munich walifunga bao mbili katika dakika mbili na kuichapa Schalke bao 2-1 na kuwapora uongozi.
Tangu rekodi yao ya kutofungwa mechi 24 kumalizwa na kipigo toka kwa Nuremberg, Bayer Leverkusen wamefifia na wamefungwa mechi yao ya 4 kati tano za mwisho walipotandikwa 3-2 na Eintracht Frankfurt na sasa wako nafasi ya 3.
Tatu Bora: Bayern Munich (pointi 59), Schalke (58), Leverkusen (53)
Tatu za mkiani: Freiburg (pointi 25), Hanover (24), Hertha Berlin (22)
Wafungaji bora: Stefan Kiessling, Kevin Kuranyi and Edin Dzeko (wote bao 18 kila mmoja), Lucas Barrios (15), Eren Derdiyok, Albert Bunjaku and Claudio Pizarro (wotel 12 kila mmoja)
La Liga: Macho yote Jumamosi
Kama ilivyotegemewa, Barcelona na Real Madrid zote zimeshinda mechi zao za wikiendi huku Barca wakiwapiga Athletic Bilbao 4-1 na Real kuichapa Racing Santander 2-0.
Matokeo hayo sasa yanaifanya, EL CLASICO, yaani ile mechi ya Jumamosi kati ya Real Madrid na Barcelona huko Bernabeau, ndio iamue nani mbabe kati ya vigogo hao na pia nani achukue uongozi wa Ligi.
Tatu Bora: Real Madrid (pointi 77, magoli +57), Barcelona (77, +56), Valencia (56)
Tatu za mkiani: Tenerife (pointi 25), Valladolid (24), Xerez (23)
Wafungaji Bora: Lionel Messi (magoli 26), Gonzalo Higuain (24), David Villa (20)
Serie A: Ngoma ngumu
Timu zote za juu zilishinda mechi zao na kufanya msimamo uwe kama ulivyokuwa kabla ya mechi za wikiendi.
Vinara Inter Milan waliichapa Bologna 3-0 kwa mabao mawili ya Thiago Motta na moja la Mario Baloteli.
AS Roma waliitungua Bari 1-0 kwa bao la Mirko Vucinic.
AC Milan walikuwa kwenye vuta ni kuvute na Cagliari na hatimae kuibuka washindi wa bao 3-2.
Tatu Bora: Inter Milan (pointi 66), Roma (65), AC Milan (63)
Tatu za mkiani: Atalanta (pointi 31), Siena (26), Livorno (26)
Wafungaji Bora: Antonio Di Natale (magoli 22), Diego Milito (18), Alberto Gilardino (15)

No comments:

Powered By Blogger