Tuesday 6 April 2010

Newcastle yarudi Ligi Kuu
Newacastle jana ilifanikiwa kuifunga Sheffield United bao 2-1 kwenye pambano la Ligi ya Coca Cola Championship na kufanikiwa kupanda Daraja kurudi Ligi Kuu ambako waliporomoka Msimu uliokwisha.
Katika mechi ya jana, Newcastle walihitaji sare tu ili wapande Daraja lakini wakajikuta wako nyuma kwa bao 1 baada ya Sheffield kupata bao dakika ya 22 kupitia Richard Creswell.
Newcastle walisawazisha kwa penalti ya Peter Lovenkrands na Kevin Nolan akapachika bao la pili na la ushindi dakika ya 73.
Meneja wa Newcastle, Chris Houghton, aliechukua wadhifa huo baada ya Kevin Keegan kubwaga manyanga, alisema ni furaha kubwa kufuzu kupanda Daraja mbele ya Mashabiki wao Uwanjani kwao St James Park lakini wanataka ushindi katika mechi zao 5 zilizobaki ili wawe Mabingwa wa Daraja hilo.
Barcelona v Arsenal
Arsenal wanaingia Nou Camp kurudiana na Barcelona baada ya kutoka sare 2-2 wiki iliyopita lakini Timu yao ina majeruhi kibao na Kiungo Alex Song ameongezeka kwenye lisi hiyo ambamo wamo Cesc Fabregas, Andrey Arshavin na William Gallas.
Barcelona nao pia watawakosa Wachezaji kadhaa wakiwemo Masentahafu wao wote wawili Carles Puyol na Gerard Pique kwa vile wana Kadi.
Vile vile Mfungaji wao mkubwa, Zlatan Ibrahimovic, yuko nje kwa kuumia lakini watamkaribisha tena Kiungo mahiri Andres Iniesta ambae amepona maumivu baada ya kuzikosa mechi kadhaa.
Katika mechi ya leo, Wenyeji Barcelona wanahitaji sare ya 0-0 au 1-1 ili wasonge Nusu Fainali wakati Arsenal wanahitaji ushindi au sare yoyote ya zaidi ya bao 2-2.
Fergie hawezi kumpanga Rooney kabla hajapona vizuri
Sir Alex Ferguson amesema hawawezi kumchezesha Wayne Rooney katika mechi ya UEFA CHAMPIONS LIGI ya Manchester United na Bayern Munich siku ya Jumatano huko OldTrafford ikiwa Mchezaji huyo hayuko fiti kwa asili mia moja.
Rooney aliumia wiki iliyopita katika mechi ya kwanza kati ya Bayern Munich na Manchester United ambayo Bayern walishinda 2-1 na Jumatano ni lazima Man United washinde ili wafuzu kuingia Nusu Fainali.
Kumekuwa na habari kadhaa katika Vyombo vya Habari kuwa Rooney atacheza mechi hiyo ya marudiano baada ya kupona haraka.
Ingawa Ferguson amegoma kumchezesha Rooney lakini alidokeza kuwa huenda akamweka benchi kwa vile Mchezaji huyo ni king’ang’anizi.

No comments:

Powered By Blogger