Friday 9 April 2010

Van Persie aanza zoezi
Straika mahiri wa Arsenal Robin van Persie karibuni atarejea uwanjani baada ya kuwa nje kwa miezi minne akiuguza enka aliyoumia mwezi Novemba akiichezea Uholanzi kwenye mechi ya kirafiki na Italia.
Van Persie tayari ameshaanza mazoezi na sasa anaweza hata kucheza mpira na anategemewa kuingia mazoezini na Kikosi cha kwanza muda si mrefu.
Vile vile, Arsenal imesema majeruhi wengine, Johan Djouroa na Kieran Gibbs, wanakaribia kuanza mazoezi.
Djourou yuko nje tangu Septemba baada ya kuumia goti na Gibbs alivunjika mfupa wa kidole cha mguu kwenye mechi ya UEFA CHAMPIONS LIGI Arsenal walipocheza na Standard Liege mwezi Novemba.
Kesho EL CLASICO ndani ya EL SANTIAGO BERNABEAU: Real Madrid v Barcelona
Ni mechi inayongojewa kwa hamu kubwa, ni mechi ambayo itaamua nani anachukua uongozi wa La Liga ‘jumla’ kwa vile Timu zote zimefungana zikiwa na pointi 77 ingawa Real ndie yuko mbele kwa tofauti ya goli moja tu.
El Clasico itachezwa El Santiago Bernabeau nyumbani kwa Real Madrid ambako Msimu uliokwisha katika mechi kama hii Barcelona iliifumua Real bao 6-2.
Katika mechi 3 za mwisho, Barca imeifunga Real mechi zote hizo ikiwemo ile ya kwanza ya La Liga Msimu huu kwa bao 1-0 ambalo Zlatan Ibrahomivc alipachika lakini safari hii huenda Ibrahimovic asicheze kwa vile ni majeruhi.
Wengi wanaitangaza mechi hii kama ni Mashindano yanayowakutanisha Wachezaji Bora Duniani Cristiano Ronaldo wa Real na Lionel Messi wa Barca na hili limepamba moto hasa baada ya Messi kuiangamiza Arsenal kwa kufunga bao zote 4 katika mechi ya Jumanne iliyopita.
Baada ya kuikosa mechi ya Arsenal kwa kuwa kifungoni, Masentahafu wa Barca, Carles Puyol na Gerrard Pique, wote watakuwepo dimbani.
Real watamkosa Supastaa Kaka ambae anauguza musuli za pajani na pia huenda Mchezaji wa zamani wa Liverpool, Xabi Alonso, asiichezee Real kwa vile ana tatizo la musuli.
KWA UFUPI TU:
-Reina asaini Mkataba mpya
Kipa wa Liverpool, Pepe Reina, amesaini Mkataba mpya na utamweka Anfield hadi 2016.
Reina, miaka 27, alijiunga na Liverpool mwaka 2005 akitokea Villareal na mpaka sasa ameshaichezea Liverpool mechi 250.
Reina alianza Soka lake akichezea Timu ya Vijana ya Barcelona na Ukipa ameurithi toka kwa Baba yake Mzazi ambae alikuwa Kipa wa Barcelona na Atletico Madrid.
-Fergie kimya kuhusu kumsajili Villa
Sir Alex Ferguson amegoma kuingizwa kwenye uvumi kuwa Manchester United imekubaliana na Straika wa Spain David Villa ajiunge nao Msimu ujao.
Man United tayari imeshasaini Wachezaji wawili kwa ajili ya Msimu ujao, nao ni Chris Smalling kutoka Fulham na Mchezaji toka Mexico Javier ‘Chicharita’ Hernandes.
Majina ambayo yamezagaa kuwa yatatua Old Trafford ni Frank Ribery, Karim Benzema na David Villa.
Ferguson ametamka: “Ni suala la kupata Mchezaji atakaetuboresha au kutufanya tusiporomoke tulipo. Huo ndio mwongozo wetu siku zote. Kila Msimu kunakuwepo uvumi. Msimu uliokwisha ni Ribery na Benzema ingawa kweli Benzema tulitoa ofa. Sasa ni David Villa! Nina hakika mpaka mwishoni mwa Msimu Majina yanayovumishwa yatafika hata nusu dazeni!”
-Sagna ataka Plani B Arsenal
Beki Bacary Sagna ameitaka Klabu yake Arsenal iwe na mkakati wa kuwa na staili ya pili pale wanaposhindwa kuzishinda Timu kwa kutmia staili yao ya ‘Soka Tamu’ ya kumiliki mpira na kupasiana hadi kwenye mstari wa golini.
Siku ya Jumanne, Arsenal walipelekwa darasani na kufundishwa jinsi ‘Soka Tamu’ linavyochezwa walipotua Uwanja wa Nou Camp na kukutana na Vigogo wa ‘Soka Tamu’ Barcelona walioongozwa na Mchawi Lionel Messi aliewafunga bao 4 mguuni mwake.
Sagna amesema: “ Nadhani kuna wakati tunamiliki na kuuchezea mpira kupindukia! Hatufikirii nini bora kwetu! Lazima tupunguze uchezaji huo na tufikirie nini kitatuletea ushindi!”
Arsenal, ambao wako pointi 3 nyuma ya vinara Chelsea kwenye Ligi Kuu, wanaitegemea Ligi wapate angalau Kikombe Msimu huu na Sagna anajipa moyo kuwa Chelsea na Man United zitapoteza pointi katika mechi 5 zilizobaki.

No comments:

Powered By Blogger