Saturday 10 April 2010

LIGI KUU LEO: Pompey washuka Daraja!!!
West Ham 1 Sunderland 0
Bila ya kucheza mechi ya Ligi Kuu na kesho wakiwa Wembley kucheza Nusu Fainali ya FA Cup kwa kuivaa Tottenham, Portsmouth leo imekuwa Klabu ya kwanza Msimu huu kuporomoka Daraja kutoka Ligi Kuu baada ya West Ham kuifunga Sunderland bao 1-0.
Bao la dakika ya 51 la Mbrazil Ilan ndilo lililowapa ushindi West Ham wakiwa nyumbani Upton Park na kuwapa pointi 3 muhimu zinazowafanya washika nafasi ya 16 wakiwa na pointi 31 kwa mechi 34.
Chini yao wapo Wigan wamecheza mechi 33 wana pointi 31 na zile Timu 3 za mkiani zilizo eneo la kushushwa Daraja ni Burnley mechi 34 pointi 27, Hull mechi 33 pointi 27 na Pompey mechi 33 pointi 14.
Vikosi vilivyoanza:
West Ham: Green, Faubert, da Costa, Upson, Spector, Stanislas, Kovac, Behrami, Noble, Cole, Ilan.
Akiba: Kurucz, Gabbidon, Franco, McCarthy, Diamanti, Daprela, Spence.
Sunderland: Gordon, Ferdinand, Da Silva, Turner, Richardson, Henderson, Meyler, Cattermole, Malbranque, Bent, Campbell.
Akiba: Carson, Bardsley, Hutton, Zenden, Jones, Kilgallon, Mwaruwari.
Refa: Michael Jones
Hull City 1 Burnley 4
Bao la kipindi cha kwanza la Martin Paterson, bao mbili za penalti za Graham Alexander na frikiki ya Wade Elliott imewafanya Burnley waibuke na ushindi wa bao 4-1 ugenini baada ya kutanguliwa kufungwa bao na Hull City alilofunga Kevin Kilbane baada ya dakika mbili tu za mchezo.
Ushindi huu umeifanya Burnley waipite Hull kimsimamo kwa tofauti ya magoli zote zikiwa na pointi sawa lakini Hull wamecheza mechi moja pungufu lakini Timu zote hizo mbili badi zipo kwenye zile Timu 3 za mwisho.
Vikosi vilivyoanza:
Hull: Myhill, McShane, Sonko, Mouyokolo, Dawson, Mendy, Boateng, Bullard, Kilbane, Fagan, Altidore.
Akiba: Duke, Barmby, Geovanni, Folan, Marney, Vennegoor of Hesselink, Cairney.
Burnley: Jensen, Mears, Duff, Cort, Fox, Alexander, Paterson, Cork, Elliott, Nugent, Steven Fletcher.
Akiba: Weaver, Carlisle, Caldwell, Blake, Bikey, Thompson, Eagles.
Refa: Martin Atkinson
WBA yarudi tena Ligi Kuu!!!
  • Waungana na Newcastle Ligi Kuu
Baada ya kuporomoshwa Daraja Msimu uliokwisha, West Bromwich Albion leo imeungana na Newcastle kupanda na kurudi Ligi Kuu baada ya kuifunga Doncaster bao 3-2 kwenye mechi ya Ligi ya Coca Cola Championship huku Ligi hiyo ikiwa bado imebakisha mechi kadhaa kumalizika.
Newcastle ndio inayoongoza Ligi hiyo ya Coca Cola Championship na ilijihakikishia kurudi Ligi Kuu wiki iliyopita na leo imekuwa zamu ya WBA ambao wanashikilia nafasi ya pili kwenye Ligi hiyo.
Timu mbili za juu za Ligi ya Coca Cola Championship ndizo zinapandishwa moja kwa moja Daraja kwenda Ligi Kuu na Timu zilizo nafasi ya 3 hadi ya 6 zinapangiwa Michuano maalum kuipata Timu moja inayoungana na Timu hizo mbili za kwanza kupanda Daraja.

No comments:

Powered By Blogger