Tuesday 6 April 2010

UEFA CHAMPIONS LIGI: Inter yaingia Nusu Fainali
Leo, Wesley Sneijder ameifungia Timu yake Inter Milan bao la frikiki dakika ya 6 na kuwashinda CSKA Moscow kwa bao 1-0 na hivyo kuihakikishia Inter inatinga Nusu Fainali kucheza na Mshindi wa mechi kati ya Barcelona na Arsenal wanaocheza baadae leo huko Nou Camp.
Mechi hii ilianza mapema, saa 1 na nusu usiku saa za bongo, katika Uwanja wa Luzhniki Jijini Moscow, Urusi na ni ya marudiano ambapo Inter Milan waliishinda CSKA Moscow pia kwa bao 1-0 wiki iliyopita lakini Mfungaji wa leo Wesley Sneijder hakucheza mechi hiyo kwa vile alikuwa majeruhi.
Licha ya kuwa na wasiwasi wa nyasi za bandia za Uwanja wa Luzhniki, Inter walionekana kutulia na kumiliki mpira vizuri katika mechi yote hiyo na wangeweza kupata mabao mengi zaidi kama wangejitutumua zaidi.
CSKA Moscow walimaliza mechi wakiwa mtu 10 baada ya Odiah kulambwa Kadi Nyekundu alipopewa Kadi za Njano mbili.
Vikosi vilivyoanza (Wachezaji walioingia na dakika waliyoingia kwenye mabano):
CSKA Moscow: Akinfeev, Semberas, Ignashevich Berezutsky, Berezutsky (Odiah 14), Shchennikov, Dzagoev, Mamaev, Gonzalez, Honda (Rahimic 77, Necid (Guilherme 71)
Inter Milan: Julio Cesar, Zanetti, Lucio, Maicon, Samuel, Stankovic, Sneijder (Muntari 86), Cambiasso, Eto'o, Milito (Balotelli 74), Pandev (Chivu 63)

No comments:

Powered By Blogger