Saturday 10 April 2010

FIFA yakamatia Watu kununua Tiketi Bondeni
FIFA imeanzisha kampeni kamambe huko Afrika Kusini ili Mashabiki wa Nchi hiyo wanunue Tiketi 500,000 ambazo hazijauzwa za mechi za Fainali za Kombe la Dunia zinazoanza Juni 11 na kwisha Julai 11.
Ni mechi ya Fainali tu ya hapo Julai 11 ambayo ndio Tiketi zote zimeuzwa.
Waandaaji wa Mashindano hayo wamekiri kuwa limefanyika kosa kutegemea mauzo kwa njia ya Mtandao katika Nchi ambayo desturi yake ni kununua Tiketi kwenye siku ya pambano.
Katibu Mkuu wa FIFA, Jerome Valckle, amesema: “Tunataka kuionyesha Dunia kuwa Viwanja vinajaa.”
Msimamizi Mkuu wa Mashindano hayo, Danny Jordaan kutoka Afrika Kusini, amesema vituo 11 katika Miji 9 itakayokuwa na mechi vimeanzishwa ili kuuza Tiketi kwenye kaunta.
Tiketi 100,000 zitauzwa kwa Watu wa Afrika Kusini kwa bei ya ‘chee’ ya Dola 20 kwa Tiketi moja kiwango ambacho ni cha chini mno kwa Viwango vya Kombe la Dunia.
Takwimu zimeonyesha USA ndio inaongoza kwa ununuzi wa Tiketi ikiwa imenunua Tiketi 118,945, Uingereza imenunua Tiketi 67,000 na Ujerumani Tiketi 32,269.

No comments:

Powered By Blogger