Thursday 8 April 2010

Man United wamsaini Chicharito!!!!
Manchester United imekamilisha usajili wa Straika kutoka Mexico, Javier Hernandez, miaka 21, ambae anatoka Klabu ya Mexico Chivas da Guadalajara ambae pia anachezea Timu ya Taifa ya Mexico.
Hernandez, aka Chicharito, atajiunga na Man United hapo Julai 1 na mkataba wake haukuanikwa ila kipengele kimoja ni Manchester United kwenda kucheza Mexico katika ufunguzi rasmi wa Uwanja mpya wa Chivas huko Guadalajara unaoweza kuchukua Watazamaji 45,000 mwishoni mwa Julai.
Bosi wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, amemsifia Mchezaji huyo mpya na kusema ni Kijana mwenye kipaji.
Chicharito huenda akaonekana Uwanjani Wembley akiichezea Mexico hapo Mei 24 itakapocheza mechi ya kirafiki na England.
Huyu ni Mchezaji wa pili kwa Man United kumsajili kwa ajili ya Msimu ujao, wa kwanza akiwa ni Sentahafu chipukizi kutoka Fulham Chris Smalling.

No comments:

Powered By Blogger