Thursday 8 April 2010

Fergie awashambulia Wachezaji Bayern!!
Sir Alex Ferguson amewashambulia vikali Wachezaji wa Bayern Munich kwa kumshinikiza Refa Nicola Rizzoli kutoka Italia ili ampe Chipukizi toka Brazil Rafael Kadi na Refa huyo kweli akamlamba Kadi ya pili ya Njano na kuifanya Manchester United icheze mtu 10 kwa dakika 40 za kipindi cha pili na kutoa mwanya kwa Bayern kupata bao muhimu la pili lililowapeleka Nusu Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI.
Ferguson alibwata mara baada ya mechi: “Kulikuwa hamna kipingamizi sisi kushinda tukiwa 11, wao walikuwa wamezidiwa! Lakini Rafael alionyesha uchanga wake na wao wakalazimisha atolewe! Kila Mchezaji wao alimkimbilia Refa- hii ni tabia halisi ya Wajerumani!”
Kuhusu kumwanzisha Wayne Rooney mechi hiyo ambayo alishindwa kuimaliza baada ya kujitonesha mguu wage na hivyo kutoka baada ya dakika 55, wakati huo huo ambapo Rafael alitolewa, Ferguson amesema hakuumia sana na atacheza mechi ijayo wikiendi hii.
UEFA CHAMPIONS LIGI: Man United & Bordeaux nje, Nusu Fainali ni Bayern v Lyon!!
Ingawa Manchester United na Bordeaux zote zilishinda mechi zao za marudiano lakini zimebwagwa nje ya UEFA CHAMPIONS LIGI kwa magoli.
Manchester United iliifunga Bayern Munich bao 3-2 na kufanya jumla ya magoli iwe 4-4 na Bayern kusonga mbele kwa idadi kubwa ya magoli ya ugenini.
Huko Ufaransa, katika mechi baina ya Klabu za Ufaransa, Bordeaux ilifanikiwa kuilaza Lyon bao 1-0 lakini ikajikuta ikitupwa nje kwa jumla ya bao 3-2.
Nusu Fainali zitakuwa ni kati ya Inter Milan v Barcelona na Bayern Munich v Lyon.

No comments:

Powered By Blogger