Saturday 10 April 2010

Fergie atoboa kuhusu Chicharita
Bosi wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, amezungumzia jinsi walivyomtambua Mchezaji kutoka Mexico, Javier Hernandez aka Chicharita, miaka 21, na kuamua kumsajili.
Ferguson amesema: “Oktoba mwaka jana tulipata ripoti zake na Skauti wetu mmoja akaenda Mexico mwezi Desemba na kutazama mechi kadhaa. Ripoti yake ilikuwa nzuri. Wakati ule tulifikiria bado ni mdogo na tusubiri lakini akachaguliwa Timu ya Taifa. Sasa tatizo likaja, je akienda Kombe la Dunia na kufanya vizuri tunaweza kumpoteza!”
Ferguson akaelezea kuwa wakaamua kumpeleka Skauti wao Mkuu, Jim Lawlor, huko Mexico na akakaa wiki 3 kumchunguza Chicharita.
Katika wiki hizo tatu, Jim Lawlor, alimshuhudia Chicharita akiichezea Timu ya Taifa ya Mexico mara mbili na Klabu yake Chivas mara moja na katika mechi zote hizo alikuwa akifunga magoli.
Ingawa Chicharita si jina linalojulikana, Ferguson amesema: “Huwa tunapenda kufanya dili kama hizi. Huwa tunavitambua vipaji na kuviendeleza. Tuna uzoefu na hilo. Na tunapenda kusajili Wachezaji wa namna hiyo!”

No comments:

Powered By Blogger