Saturday 3 April 2010

Chelsea washika hatamu!
  • Man United 1 Chelsea 2
  • Arsenal 1 Wolves 0
Chelsea leo wameifunga Manchester United Uwanjani Old Trafford bao 2-1 na kushika uongozi wa Ligi Kuu wakiwa na pointi 74, wakifuata Man United pointi 72 na Arsenal pointi 71.
Mabao ya Chelsea yalifungwa na Joe Cole na Drogba na lile la Man United alifunga Kiko Macheda.
Hata hivyo baada ya mechi, Meneja Msaidizi wa Man United Mike Phelan alilalamikia uamuzi na wengi waliona bao la pili la Chelsea likifungwa na Drogba akiwa wazi wazi ofsaidi.
Katika mechi iliyofuata baadae, Arsenal walimudu kupata bao dakika ya mwisho ya mchezo Mfungaji akiwa Niklas Bendtner na kuishinda Wolves bao 1-0.
MATOKEO KAMILI:
Arsenal 1 Wolves 0
Bolton 0 Aston Villa 1
Man Utd 1 Chelsea 2
Portsmouth 0 Blackburn 0
Stoke 2 Hull 0
Sunderland 3 Tottenham 1
MSIMAMO:
[Kwa Timu za juu]
1 Chelsea mechi 33 pointi 74
2 Man United mechi 33 pointi 72
3 Arsenal mechi 33 pointi 71
4 Tottenham mechi 32 pointi 58
5 Man City mechi 32 pointi 57
6 Liverpool mechi 32 pointi 54

No comments:

Powered By Blogger