Friday 2 April 2010

West Ham walalamika Ligi Kuu kuhusu Fulham
• Ni kwa kupanga Timu dhaifu dhidi ya Hull City
Wasimamizi wa Ligi Kuu wamethibitisha kupokea malalamiko ya West Ham kuhusu uamuzi wa Meneja wa Fulham, Roy Hodgson, wa kupanga Kikosi dhaifu dhidi ya Hull City Jumamosi iliyopita kilichofungwa na Hull City bao 2-0.
Ushindi huo wa Hull City, ambao ni moja ya Timu 3 zilizo mkiani, uliifanya Hull iwe sawa kwa pointi na West Ham zote zikiwa na pointi 27 ingawa West Ham wako juu kwa idadi ya magoli.
Hogson aliwapumzisha Wachezaji Bobby Zamora, Danny Murphy, Damien Duff, Aaron Hughes na Dickson Etuhu katika mechi hiyo na Hull lakini wote walirudi Kikosini Fiulham ilipoifunga Wolfsburg 2-1 kwenye EUROPA LIGI Alhamisi Aprili 1.
Msemaji wa Ligi Kuu amethibitisha kupokea malalamiko ya West Ham na amesema wao watawasiliana na Fulham ili kupata maoni yao kisha Bodi ya Ligi Kuu itakaa kutoa uamuzi.
Sheria za Ligi Kuu zinatamka kila Timu inatakiwa kupanga Kikosi chao bora kilichopo wakati huo.
Wakipatikana na hatia, Fulham wanaweza kupigwa Faini ya Pauni 25,000 sawa na Wolves ambao walipatikana na hatia ya kupanga Kikosi dhaifu walipocheza na Manchester United Septemba mwaka jana.
Kocha wa Wolves, Mick McCarthy, aliwapumzisha Wachezaji 9 kati mechi hiyo na Man United.
Hata hivyo,Hodgson amesisitiza Fulham haikufanya kosa lolote na amesema yeye atakuwa akibadilisha Wachezaji ikibidi.
Hodgson ametamka: “Hakika, West Ham hawatakiwa kutupangia Timu! Sisi hatuna kesi ya kujibu! Tulipocheza na Hull, nilimpanga Mchezaji ambae kauzwa Pauni Milioni 10 kwa Man United [akimaanisha Chris Smalling], Kagisho Dikgacoi, ni Mchezaji wa Kimataifa wa Afrika Kusini na nilimbadili Zamora kwa kumchezesha Dempsey ambae ni Mchezaji wa Kimataifa wa USA!”
Hodgson aliongeza kwa kusema Liverpool, Man United na Chelsea zikibadili Wachezaji hakuna anaelalamika.
Nae Meneja wa Wigan, Roberto Martinez, amemsapoti Hodgson kwa kuiita hatua West Ham kuishtaki Fulham ni upuuzi.

No comments:

Powered By Blogger