Wednesday 31 March 2010

Wenger hatishiki na Barca
Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, amesema wao hawaiogopi Barcelona ambayo leo wanapambana nayo Uwanja wa Emirates kwenye mechi ya kwanza ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE.
Wenger ametamka: “Lazima tuwe Mashujaa na kupigana! Unachotaka toka Timu yako ni kutojali ubora wa Barcelona na kukazania ubora wetu! Ni kweli wao ni Timu nzuri lakini hata sisi ni Timu bora!”
Barcelona ni tishio hasa kwa vile wanae mmoja wa Wachezaji bora duniani, Lionel Messi, anaesaidiwa na kina Zlatan Ibrahimovic, Andreas Iniesta, Xavi na Mchezaji wa zamani wa Arsenal, Thiery Henry.
Katika mechi ya leo huenda Arsenal wakamkosa Nahodha wao, Cesc Fabregas, ambae ni majeruhi ingawa upo uwezekano mdogo akacheza.
Lisi ya FIFA ya Ubora Duniani: Spain vinara, Brazil wa pili na Bongo ni 108!!!
Katika Listi ya FIFA ya Ubora Duniani kwa mwezi huu iliyotolewa leo, Spain bado nambari wani, Brazil ni wa pili, Uholanzi ni nambari 3 na England ni wa 7.
Tanzania ipo nafasi ya 108 na imeporomoka nafasi 2.
Timu ambayo imepata mafanikio makubwa ni Senegal iliyopanda nafasi 22 na kushika ya 72.

No comments:

Powered By Blogger