Thursday 1 April 2010

Fabregas nje Msimu wote!!
Nahodha wa Arsenal Cesc Fabregas ataukosa Msimu wote uliobaki baada ya kuvunjika mfupa wa mguu wake katika mechi ya UEFA CHAMPIONS LIGI siku ya Jumatano Uwanjani Emirates Arsenal walipotoka droo ya 2-2 na Barcelona.
Fabregas alivunjika mguu huo alipogongana na Carles Puyol na kupata penalti kwa tukio hilo.
Uchunguzi wa Madaktari umethibitisha Fabregas anahitaji si chini ya wiki 6 ili kupona na Msimu wa Ligi Kuu unakwisha Mei 9.
Mchezaji mwingine wa Arsenal ambae huenda akawa nje hadi Msimu unakwisha ni Beki William Gallas ambae alijitonesha musuli ya mguu ambayo ilimweka nje kwa muda mrefu kabla ya kucheza mechi hiyo na Barcelona na kujiumiza tena.
Pia, inasemekana Fowadi Andrey Arshavin, ambae pia aliumia kwenye mechi na Barcelona, huenda akawa nje muda mrefu ingawa ufafanuzi haukutolewa.
Rooney hakuumia sana! 
Mshambuliaji wa England Wayne Rooney atakuwa fiti kucheza Fainali za Kombe la Dunia baada ya uchunguzi wa Madaktari kuthibitisha hakuvunjika mfupa na wala hakuumia vibaya sana.
Habari hizo zimetolewa na Klabu yake Manchester United ingawa ufafanuzi zaidi haukutolewa na inategemewa Meneja wa Klabu hiyo, Sir Alex Ferguson, atazungumzia suala la Rooney kesho Ijumaa.
Rooney aliumia kwenye mechi ya UEFA CHAMPIONS LIGI huko Ujerumani ambako Bayern Munich waliifunga Man United bao 2-1 siku ya Jumanne.
Baada ya kuumia Rooney England yote ilikuwa na wasiwasi kuwa Mchezaji huyo huenda ameumia vibaya na hivyo kuikosa Fainali ya Kombe la Dunia itakayoanza Juni 11.
Msimu huu Rooney ameifungia Manchester United bao 34 na pia amefunga bao 9 kwa England katika mechi za mchujo za Kombe la Dunia.

No comments:

Powered By Blogger