Wednesday 31 March 2010

Mourinho achoshwa na Wataliana!
Meneja machachari na mwenye vituko na mbwembwe, Jose Mourinho, ameibua mjadala kuhusu hatima yake katika Soka la Italia baada ya kutamka kuhusu Soka huko Italia: “Silipendi na halinipendi”
Mourinho, ambae ni Meneja wa Inter Milan, amegoma kuongea na Waandishi wa Habari baada ya kupigwa Faini Pauni 35,000 na kufungiwa na Chama cha Soka cha Italia kwa kuwakandya Marefa.
Mourinho amesema: “Nina furaha na Inter lakini sina furaha na Soka la Italia!”
Mourinho, miaka 47, ameongeza: “Siku zote nazungumza toka moyoni lakini nikizungumza yaliyo moyoni kuhusu Soka ya Serie A watanifungia!’
Inter Milan leo usiku inacheza na CSKA Moscow kwenye mechi ya kwanza ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI na kwenye hatua iliyopita Inter waliibwaga Klabu ya zamani ya Mourinho, Chelsea.
Kuna uvumi mkubwa kuwa Mourinho yuko mbioni kurudi Uingereza kuiongoza mojawapo ya Klabu za Ligi Kuu ingawa si Klabu yeyote wala yeye mwenyewe aliethibitisha hilo.
Rooney nje wiki 4!
Wayne Rooney huenda akawa nje ya uwanja kwa wiki hadi nne baada ya kuteguka enka kwenye mechi ya jana ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI ambayo Manchester United walifungwa na Bayern Munich bao 2-1 kwenye Uwanja wa Allianz Arena huko Munich, Ujerumani.
Ingawa inasemekana maumivu ya Rooney si makubwa sana na ya kutisha lakini ni wazi atazikosa mechi za Man United na Chelsea ya Ligi Kuu siku ya Jumamosi na marudio ya Man United na Bayern Munich Jumatano ijayo.

No comments:

Powered By Blogger