Monday 29 March 2010

LIGI KUU leo: Man City v Wigan
• Adebayor kuwa na Tevez!
Straika wa Manchester City Emmanuel Adebayor leo anarudi uwanjani baada ya kutumikia kifungo chake cha mechi 4 na Kocha Roberto Mancini amesema atampanga acheze pamoja na Carlos Tevez ili kuleta nguvu mbele na kupata ushindi dhidi ya Wigan katika mechi ya Ligi Kuu leo Uwanjani City of Manchester.
Man City walipoteza mechi yao ya mwisho ya Ligi walipofungwa na Everton 2-0 hapo hapo nyumbani Uwanjani City of Manchester.
Mwaka huu, Tevez na Adebayor wamecheza pamoja mara 3 tu kati ya mechi 17 ambazo wangeweza kuwa pamoja kwa vile kwanza Adebayor alikuwa Angola kwenye Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika kisha Tevez akapata udhuru wa kifamilia na kurudi kwao Argentina na aliporudi tu, Adebayor akafungiwa mechi 4 baada ya kutolewa kwa Kadi Nyekundu katika mechi na Stoke City.
Man City, pamoja na Tottenham, Liverpool na Aston Villa, wamo kwenye vita kati yao kuwania nafasi ya 4 ili kufuzu kucheza UEFA msimu ujao.
Tottenham ndie yuko nafasi hiyo ya 4 akiwa na pointi 58 kwa mechi 31, anafuata Liverpool mwenye pointi 54 kwa mechi 32, kisha Man City pointi 53 mechi 30 na wa 7 ni Aston Villa mwenye pointi 51 kwa mechi 31.
Vidic akwepa rungu la FA!
Beki wa Manchester United hatachukuliwa hatua yeyote na FA kufuatia tukio la yeye kumpasua kwa kiwiko Mchezaji wa Bolton Johan Elmander siku ya Jumamosi Man United ilipoifunga Bolton 4-0.
FA imethibitisha uamuzi huo kwa sababu Refa Martin Atkinson aliliona tukio hilo na kuamua ni bahati mbaya.
Meneja Bolton Owen Coyle alidai Elmander aliumizwa kusudi.

No comments:

Powered By Blogger