Sunday 28 March 2010

Injini ya Barca nje mechi na Gunners!!
Kiungo mahiri wa Barcelona Andres Iniesta ataikosa mechi ya UEFA CHAMPIONS LIGI Barca watapokuwa Uwanja wa Emirates kucheza na Arsenal siku ya Jumatano Machi 31 baada ya kuumia paja Jumamosi katika mechi ya La Liga ambayo Barcelona waliifunga Real Mallorca bao 1-0.
Ilibidi Iniesta atolewe nje mapema kipindi cha pili na nafasi yake kuchukuliwa na Lionel Messi aliepumzishwa kwa mechi hiyo.
Uchunguzi wa Madaktari umebaini Iniesta anatakiwa awe nje kwa siku 10.
Barcelona wataikaribisha Arsenal Nou Camp kwa mechi ya marudiano hapo Aprili 6.
Ribery na Robben ndio nguvu ya Bayern!!
Sir Alex Ferguson amesema Franck Ribery na Arjen Robben ndio tishio kubwa kwa Manchester United watakapoikwaa Bayern Munich siku ya Jumanne Uwanja wa Allianz Arena huko Ujerumani katika mechi ya kwanza ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI.
Ingawa Ferguson amekiri Ribery ni kipaji lakini amesema hawezi kuwapata Wayne Rooney na Lionel Messi.
Kuhusu Robben, Ferguson amesema Winga huyo ambae ni Mdachi ni hatari kwani hucheza Winga ya kulia ingawa mguu wake bora ni wa kushoto hivyo akipenya kuingia kati huachia mikwaju na guu lake la kushoto.
Hata hivyo, Ferguson amesema anaamini anao Mafulbeki wazuri wanaoweza kumdhibiti Robben.
Akikumbushia Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI ya mwaka 1999 Manchester United walipoibwaga Bayern Munich 2-1 na bao zote hizo mbili zikifungwa katika dakika3 za nyongeza za majeruhi, Fergie amesema: “Ile ilikuwa Fainali kiboko! Haiwezekani ikatokea tena! Kila wakati Timu ikiwa mbele 1-0 na zimebaki dakika 3 wataikumbuka Man United! Tulishindaje? Hata leo sijui, ni kudra tu! Lakini usisahau, Timu ile ilikuwa ikifunga magoli mengi mwaka ule dakika za majeruhi sasa hilo si bahati tu! Lakini ukiwa nyuma 1-0 na Refa wa Akiba anainua bango kuashiria dakika 3 za nyongeza, huwezi ukategemea utashinda mechi!”

No comments:

Powered By Blogger