Tuesday 30 March 2010

Bayern 2 Man United 1
Bayern Munich wakiwa kwao Allianz Arena wameifunga Manchester United bao 2-1 katika Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI.
Man United ndio waliokuwa wa kwanza kupata bao dakika ya pili tu baada ya frikiki ya Nani kuparazwa na Beki wa Bayern kwa kichwa na kumkuta Wayne Rooney aliefunga kifundi.
Bayern walisawazisha kwenye dakika ya 77 baada ya frikiki ya Frank Ribery kumbabatiza Rooney na kumbabaisha Kipa Van der Sar.
Huku mechi ikielekea kuwa sare, Bayern walipata bao dakika ya mwisho Mfungaji akiwa Ivica Olic.
Timu hizi zitarudiana Old Trafford Aprili 7.
Vikosi vilivyoanza:
Bayern Munich: Butt, Lahm, Van Buyten, Demichelis, Badstuber, Altintop, Van Bommel, Pranjic, Ribery, Muller, Olic
Man United: Van der Sar, Neville, Evra, Ferdinand, Vidic, Nani, Carrick, Fletcher, Schole, Park, Rooney
Refa: Frank De Bleeckere [Ubelgiji]
Lyon 3 Bordeaux 1
Lyon wameanza vyema Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI baada ya kuwafunga Wafaransa wenzao Bordeaux bao 3-1 Uwanjani Stade Gerland.
Marudio ni Aprili 7.
Vikosi vilivyoanza:
Lyon: Lloris, Reveillere, Cris, Bodme, Cissokho, Makoun, Toulalan, Delgado, Pjanic, Michel Bastos, Lopez.
Bordeaux: Carrasso, Chalme, Sane, Ciani, Tremoulinas, Gouffran, Plasil, Menegazzo, Wendell, Gourcuff, Chamakh.

No comments:

Powered By Blogger